Rugemarila ataka mwizi bilioni 309 abainishwe...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abdulrahim Sadiki
JAMES Rugemarila  anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji wa fedha ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa anahitaji ushirikiano baina yake na upande wa mashtaka ili kubaini mwizi wa bilioni 309  za serikali.

James Rugemarila wa kwanza kushoto

Ameyasema hayo leo umbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi baada ya Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Leornad Swai kudai kesi hiyo ilipangwa kwa ajili  ya kutajwa na upelelezi wake bado haujakamilika.

Pia Rugemarila amedai hajawahi kupata nafasi ya kuzungumza na mawakili wake tangu alipotoka mahakama tarehe iliyopita.

Hivyo anashindwa kupata ushauri, wala hajui nini kinaendelea kuhusu kesi yake, hivyo ameomba waruhusiwe mawakili wawili badala ya kumi ili wawe wanamuelezea kuhusu mwenendo wa kesi.

Awali kabla ya kutoa hoja hizo, wakili wa utetezi Balomi amedai  suala la upelelezi katika kesi hiyo linachelewesha na kuwa linakiuka misingi ya haki ya kikatiba kwa washtakiwa.

Balomi amedai kuwa ni miezi 6 sasa, tunaambiwa upelelezi haujakamilika, Wakili wa serikali anashindwa hata kutuambia umefikia wapi na umebaki muda gani kukamilika.

Pia wakili Balomi amedai hali ya washtakiwa kiafya sio nzuri hasa Sethi, hivyo upelelezi ukamilishwe kwa haraka ama wawe wanaelezwa hatua ulipofikia.

Akijibu hoja hizo Wakili Swai alidai upande wa utetezi ndio umekuwa ukikwamisha mchakato wa upelelezi kwani wamekuwa wakiwanyima baadhi ya nyaraka.

Swai amedai kuwa anashukuru wanaelewa kwamba upelelezi ni mchakato na katika kuonyesha hilo wiki iliyopita walifanya mahojiano na washtakiwa licha ya kuwa mshtakiwa Seth aliwanyima ushirikiano.

Pia Swai amedai kuwa kuchelewa kwa upelelezi huo kunasababishwa na ushahidi mwingine kuwepo nje ya nchi.
Baada ya kueleza hayo, Hakimu Shaidi aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 22, 2017 ambapo ameutaka upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi.
Mbali ya Rugemarila, mshtakiwa mwingine ni Harbinder Singh Sethi ambapo wanakabiliwa na mashtaka 12 ya  uhujumu uchumi, utakatisha fedha  na kuisababisha serikali hasara ya USD 22, 198,544.60 na bilioni 309

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search