Mjema:Ukimwi changamoto kufikia sera ya viwanda...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Salha Mohamed 

MKUU wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amesema janga la Ukimwi bado ni changamoto katika kufikia sera ya viwanda nchini.
Mkuu wa wilaya Ilala Sophia Mjema akihutubia wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani jijini Dar es Salaam.

Mjema ameyasema hayo jana wakati wa kelele cha siku ya ukimwi duniani. 

Amesema janga hilo ni matokeo ya mchanganyiko wa sababu nyingi za kibaiolojia, Kijamii, kimila na kiuchumi. 

"Madhara ya Ukimwi yameadhiri watu binafsi familia na jamii kwa ujumla hivyo udhibiti wake unahitaji nguvu za pamoja za wananchi na wadau wa maendeleo, asasi za kiraia, sekta binafsi, taasisi za dini na serikali, "amesema. 

Amesema mkoa wa Dar es Salaam ni miongoni mwa mikoa yenye changamoto nyingi katika kukabiliana na maambukizi ya Ukimwi. 

Mjema amesema mkoa huo umekuwa na mwingiliano mkubwa wa watu kutoka ndani na nje ya nchi kwa ajili ya shughuli mbalimbali. 

Amefafanua kuwa mbali na mwingiliano huo, kiwango cha maambukizi kimeendelea kushuka kutoka asilimia 9.3 hadi asilimia 6.9 kwa mwaka 2007 hadi 2012.

"Haya ni mafanikio makubwa ya kujivunia. Hatutakiwi kubweka na mafanikio haya na kujisahau kwani kunaweza kusababisha kiwango hiki cha maambukizi kupanda tena, "amesema. 

Ameongeza kuwa jitahidi zinatakiwa kuchukuliwa ili maambukizi yaendelee  kushuka ili kufikia lengo la kumaliza kabisa ukimwi ifikapo 2030.

Mjema ametoa wito kwa wananchi wa mkoa huo kuchukua tahadhari na kuepuka maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi na kufika 0 mkoani humo na kujiepusha na tabia hatarishi. 

"Hadi Oktoba 2017 watu waliopima virusi vya ukimwi na kupokea majibu ni milioni 1.3, wanaume 52953 sawa na asilimia 37 na wanawake 87770 sawa na asilimia 63,"amesema.

Amesema waliogundulika kuwa na maambukizi ya virusi walikuwa 42695 ambapo wanaume ni 16950 sawa na asilimia 40, wanawake wakiwa 25745 sawa na asilimia 60.
Amesema jumla ya maambukizi kwa mkoa huo ni asilimia 3.0 ukilinganisha na takwimu za mwaka 2011/2012 inaonesha kupungua kwa maambukizi mapya. 

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana na ajira,  Jenista Mahagama amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya kudhibiti Ukimwi(TACAIDS) , Dk.  Leonard Maboko kuanzisha kampeni maalumu ya wanaume kupima ukimwi hapa nchini 2018. 

"Bado kunatatizo la mwitikio wa wanaume kujitokeza na kupima virusi vya ukimwi... Mwaka 2018 namuagiza aandae kampeni maalumu ya kuwahamisisha wanaume wote kupata nafasi ya kupima virusi vya ukimwi, "amesema . 

Amesema itasaidia kuendelea na mwitikio wa mapambano ya ukimwi huku akiwasihi wanawake kuendelea kuwa mstari wa mbele kupima na kujua afya zao. 


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search