Mkuu wa wilaya aonya wafanyabiashara....soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu
MKUU wa wilaya ya Mbeya, Poul Ntinika ameonya  wafanyabishara wanaokaidia agizo la serikali  la  kuendelea kuuza pombe na vyakula kwa kujificha kufuatia kufungiwa kutokana na kuwapo  kwa ugonjwa wa kipindupindu.


Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Poul Ntinika (kulia) akinunua ndizi kutoka kwa mfanyabishara  ambaye akutaja jina lake katika soko la Maghorofani kata ya Uyole (kushoto) Mkuu wa Mkoa wa Mbeya ,Amos Makalla.

Ntinika amesema  walilazimika kufunga biashara kwenye  vilabu vya pombe za kienyeji na mama lishe kufuatia kuwapo kwa mgonjwa aliyekuwa na   dalili za kipindupindu.
Kata zinazokabiliwa na changamoto hiyo ni  Mbalizi road, mabatini, simike na mamlaka ya mji mdogo wa Mbalizi.

"Watu hawaelewi kuna dalili za kuwepo ugonjwa wa kipindupindu na tumebaini kuna wafanyabishara wanakaidi agizo la serikali sasa nimewaagiza watendaji ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao."amesema

Ntinika amewataka wananchi  kuzingatia kanuni za afya ili kujikinga na magonjwa  yanayoepukika na  kuboresha afya zao.

Diwani wa kata ya Mbalizi Road, Adam Hussein, (CCM) amewataka wananchi kuunga mkono jitihada za serikali kwa kuzingatia kanuni bora za afya

Mwenyekiti wa mtaa wa Mwasyoge kata ya Mbalizi road, Noah Mwakafwila amesema zoezi la kufuatilia wafanyabishara wanaouza vyakula na  pombe kwa siri litaanza.

Amesema sera ya usafi  ni kipaumbele chake na kwamba kila kaya inawajibu wa kutekeleza hilo.


Hata hivyo mfanyabishara wa vileo, Sarah Braison ameiomba serikali kuwafungulia kwa kuwa idadi kubwa wanamikopo na sasa wanakosa  fedha za  marejesho hali inayoweza kukimbia na kutelekeza familia zao.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search