Mwakyembe kushuhudia Simba ikipata mmiliki mpya ...soma habari kamili na matukio360..#share
Na mwandishi wetu
WAZIRI wa Habari, utamaduni, Sanaa na michezo Dk. Harrison Mwakyembe kesho anatarajia kushuhudia klabu ya Simba ikiweka historia pale itakapomtangaza mzabuni aliyeshinda kuimiliki kwa asilimia 51.
Kikosi cha Simba Sc.
Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo imesem kuwa Dk. Mwakyembe anatarajia kuwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu ambao utamtangaza mshindi wa umiliki wa klabu.
"Simba SC imekuwa na sifa nyingi ndani na nje ya uwanja. Moja ya sifa kuu ya Simba SC ni uwezo wa wanachama, mashabiki na wapenzi wake kukubaliana na mabadiliko chanya,"
"Ikiwa imeanza mchakato wa ubadilishaji wa uendeshaji na umiliki, kesho ni siku kubwa kwa Simba ambapo mzabuni aliyeshinda kumiliki sehemu ya klabu hii atatajwa kwenye Mkutano Mkuu maalum," imesema.
Mkutano huu utaonyeshwa live kwenye kurasa za Simba SC
WAZIRI wa Habari, utamaduni, Sanaa na michezo Dk. Harrison Mwakyembe kesho anatarajia kushuhudia klabu ya Simba ikiweka historia pale itakapomtangaza mzabuni aliyeshinda kuimiliki kwa asilimia 51.
Kikosi cha Simba Sc.
Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo imesem kuwa Dk. Mwakyembe anatarajia kuwa mgeni rasmi katika mkutano mkuu ambao utamtangaza mshindi wa umiliki wa klabu.
"Simba SC imekuwa na sifa nyingi ndani na nje ya uwanja. Moja ya sifa kuu ya Simba SC ni uwezo wa wanachama, mashabiki na wapenzi wake kukubaliana na mabadiliko chanya,"
"Ikiwa imeanza mchakato wa ubadilishaji wa uendeshaji na umiliki, kesho ni siku kubwa kwa Simba ambapo mzabuni aliyeshinda kumiliki sehemu ya klabu hii atatajwa kwenye Mkutano Mkuu maalum," imesema.
Mkutano huu utaonyeshwa live kwenye kurasa za Simba SC
No comments:
Post a Comment