Serikali yataja siri kumi kufanikiwa katika ujasiliamali ...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Salha Mohamed, Dar es Salaam

KATIBU tawala mkoa wa Dar es Salaam(RAS),Theresia Mbando ametoa siri kumi kwa wajasiliamali kufanikiwa na kukuza uchumi nchini. 

Katibu tawala(RAS) mkoa wa Dar es Salaam,Theresia Mbando akiangalia moja ya bidhaa zilizotengenezwa na wajasiliamali  jijini Dar es Salaam.

Ameyasema hayo alipokuwa akifunga mafunzo ya siku tano kwa wakufunzi na wajasiliamali 73 kutoka mikoa mbalimbali ikiwamo Tanga, Njombe, Morogoro, Shinyanga, Singida na Dar es Salaam yaliyotolewa na Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO).

Amesema miongoni mwa siri hizo ni ujasiri wa kuthubutu na kuchukua tahadhari ya kupata hasara bila kukata tamaa.

Ya pili ni  malengo ya muda mrefu na mfupi yatakayowaongoza katika utendaji na  sababu ya tatu ni kutafuta na kufuata  taarifa zinazohusu ujuzi.

"Mkazalishe wajasiliamali na kutengeneza bidhaa bora ili zikidhi viwango vya soko la ndani na nje,"amesema.

Katibu tawala huyo amesema sababu ya  tano ni  kufanya biashara kwa kujiamini na kutafuta mianya iliyowazi kwa wateja. Sababu ya sita kuheshimu mikataba ya kazi kwa wateja inayoendana na bidhaa zao.

Sababu ya saba ni kuwa na uwezo wa kushawishi wateja na si kumwona mteja anashida. Ya  nane  uvumilivu.

"Sababu ya tisa ni  mtengeneze bidhaa zinazokidhi matarajio ya walaji hii itasaidia kuwaongezea kipato, "amesema.

Amesema wajasiliamali wanapaswa kupokea ushauri kutoka kwa wateja, wataalam na kuifanyia kazi na kuendesha biashara katika mfumo rasmi ili kuepusha hasara.

Amesema mbali na siri hizo wanapaswa kufuata utaratibu na matakwa ya serikali kuwa na leseni pamoja na kuthibitishwa na shirika la viwango (TBS).

Meneja wa SIDO mkoani Dar es Salaam, MacDolnard Maganga amewaasa wajasiliamali  kuweka vifungashio vinavyovutia ili kuvutia wateja.


"Kama kifungashio si kizuri hakina mvuto hakuna mnunuzi atakayenunua ni lazima viwe na ubora, "amesema. 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search