Waarabu wamtunishia misuli Donald Trump....soma habari kamili na matukio360...#share

Na mashirika ya kimataifa
WAZIRI wa mashauri ya nchi za kigeni wa Lebanon, Gebran Bassil amesema  mataifa ya kiarabu, yanafaa kufikiria hatua ya kuiwekea Marekani vikwazo vya kiuchumi ili kuizuia kuhamishia makao makuu ya Israeli hadi Jerusalem, kutoka Tel- Aviv.

Pia Bassil amesema hatua za kidiplomasia na kisiasa, zinafaa kuchukuliwa, kisha kufuatiwa na vikwazo vya kiuchumi na kifedha.

Rais wa Marekani, Donald Trump

Ametoa msimamo huo katika mkutano wao mjini Cairo-Misri.

Taarifa walioitoa kwa kauli moja kwenye mkutano wao Mjini Cairo- Misri, muungano huo wa waarabu umesema kuwa hatua ya Marekani  kuutambua mji wa Jerusalem kama makao makuu ya Israel ni hatari na ni ukiukaji wa sheria za kimataifa, na litaitumbukiza mataifa ya mashariki ya kati katika ghasia mbaya.

Mawaziri kwenye mkutano huo, sasa wanaiomba jamii ya kimataifa kutaja Mashariki mwa Jerusalem kama makao makuu ya Palestina.


Kumeshuhudiwa tena ghasia katika ukanda wa Gaza na maeneo ambayo yanashikiliwa na Israeli, Magharibi mwa mto Jordan.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search