Watoto sita wapelekwa Israel kutibiwa moyo...soma habari na matukio360..#share

Na Mwandishi Wetu

TAASISI ya moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Taasisi ya okoa moyo wa mtoto (Save a Child’s  Heart – SACH) ya nchini Israel zimewapeleka  watoto sita wenye umri wa mwaka mmoja hadi  miaka kumi na tatu  nchini Israel kwa ajili ya matibabu ya moyo.

Taarifa iliyotolewa leo na kitengo cha uhusiano na masoko cha JKCI, imesema watoto hao wamesafiri jana alifajiri wakiwa na wazazi wao pamoja na  wauguzi.

Baada ya matibabu ya watoto kukamilika  maafisa wauguzi wawili watabaki kwa ajili ya kuhudhuria mafunzo ya mwaka mmoja ya jinsi ya kuwahudumia wagonjwa waliopo katika wodi ya uangalizi maalum (ICU) na chumba cha upasuaji.

Taasisi  yetu inatibu magonjwa mbalimbali ya moyo kwa watoto  kupitia  wataalamu wazalendo tulionao. Hata hivyo tunamkataba na Israel kwa baadhi ya wagonjwa wachache wanaohitaji utaalamu wa juu zaidi kuwapeleka nchini humo kwa ajili ya matibabu,” imesema.

Tunaushirikiano mzuri na nchi ya Israel kwani gharama za matibabu ya watoto hawa zinagharamiwa na SACH. Licha ya Maafisa Wauguzi wawili kubaki nchini humo kwa ajili ya kuhudhuria mafunzo pia tuna madaktari bingwa wa magonjwa ya moyo sita   na wauguzi wawili ambao wamesoma nchini Israel na hivi sasa wanatibu wagonjwa katika taasisi yetu,”.

Daktari mmoja wa JKCI bado anaendelea na masomo nchini humo.

Hilo ni kundi la tano  la watoto kwenda kutibiwa magonjwa ya moyo nchini Israel tangu mwaka 2015 ambapo JKCI ilianza ushirikiano  na taasisi ya okoa moyo wa mtoto (Save a Child’s Heart –SACH)  ya kuwapeleka wagonjwa nchini humo.

Hadi sasa watoto 46 wameshatibiwa nchini humo na wanaendelea vizuri.

Taasisi imeendelea kutoa wito kwa wazazi na walezi kupima afya za watoto wao ili kuweza kubaini kama kuna hali ya tofauti katika ukuaji wa mtoto kwani magonjwa mengi ya moyo yanaanzia utotoni.


Mtoto akianza kuuguwa magonjwa ya moyo wazazi wengi wanadhani ni matatizo ya kifua baada ya kumfikisha mtoto Hospitali na kufanyiwa vipimo  ndipo inagundulikwa kuwa mtoto anasumbuliwa na magonjwa ya moyo.





About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search