Wakala serikali mtandao yataja mafanikio kumi....soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

WAKALA wa Serikali Mtandao kutoka Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, umeeleza mafanikio kumi ya utekelezaji wa serikali mtandao kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Mkurugenzi Mtendaji wa Wakala ya Serikali Mtandao Dk. Jabiri Bakari, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Serikali Mtandao Dk. Jabiri Bakari amesema “Ndani ya miaka mitano, serikali imeijengea uwezo wa wakala ulioiwezesha kutekeleza jitihada a serikali mtandao kwa kusaidia kusogeza huduma za taasisi za serikali karibu na umma,”.

Dk. Bakari ametaja mafanikio hayo kuwa ni kusimamia utekelezaji wa viwango na miongozo ya serikali mtandao kwa taasisi za umma ili kuwezesha utekelezaji wa serikali mtandao, zaidi ya hayo, wakala inatumia viwango na miongozo hiyo kutoa maelekezo ya namna sahihi ya kutekeleza jitihada za serikali mtandao na kupunguza urudufu.

Kuendesha vituo vya kuhifadhi mifumo na data zaa serikali vinavyotoa huduma za kuhifadhi tovuti, mifumo tumizi, utunzaji katika sehemu zaidi ya moja,“ co-locatio” na usajili na uhifadhi wa majina miliki.

Kutengeneza na kuendesha mtandao wa mawasiliano serikalini (GovNet) ulio salama na nafuu ambao taasisi za umma 150 zikiwemo Wizara na Idara za serikali, hospitali za mikoa na baadhi ya Ofisi za halmashauri.

Mengine ni kutoa huduma za ushauri kwa taasisi za umma 299 na huduma za msaada wa kiufundi 2947 katika maeneo ya uhakiki wa mifumo ya Tehama, tathmini ya usalama wa Tehama, utengenezaji wa mpango wa kukabili majenga, utayarishaji wa mkakati wa Tehama, utayarishaji wa sera ya Tehama, na utayarishaji wa usanifishaji wa shughuli na uhakiki wa miradi ya Tehama.

 Kutoa mafunzo ya kiufundi ya serikali matandao katika maeneo ya, usimamizi wa mtandao kwa taasisi 240, mfumo wa baruapepe serikali kwa taasisi 359, utekelezaji wa huduma mtandao kwa taasisi 76 na usimamizi wa tovuti kwa taasisi 411.

Kuhuisha na kusanifu upya tovuti ya serikali kuwa tovuti kuu ambayo ni kituo kimoja cha kutolea taarifa na huduma mtandao kwa wananchi kwa kupitia sehemu ya huduma za simu za mkononi na wavuti ya tovuti hiyo.

Kutengeneza na kuendesha mfumo wa huduma za serikali kwa kutumia simu za mkononi (mGOV) kama kituo kimoja cha huduma zote za serikalini kwa simu za mkononi ambapo jumla ya taasisi za umma 117 zinatumia mfumo huo na zaidi ya miamala 15 milioni imefanywa.

Ameongeza, mfumo wa ofisi mtandao (GeOS) ulisanifiwa, kutengenezwa na kutumika kuwezesha shughuli za kila siku za umma. Kwa sasa taasisi n za umma 28 zimeunganishwa na kutumia mfumo huu.

Mfumo wa Serikali wa baruapepe (GMS) ulisanifiwa, kutengenezwa na kutumika, kuwezesha mawasiliano ya ofisi ambapo jumla ya taasisi za umma 359 zikiwemo  ofisi za ubalozi zimeunganishwa na zinatumia mfumo huu.

Na Wamewezesha usanifu na utekelezaji wa mifumo mbalimbali inayowezesha utendaji kazi katika taasisi za umma ikiwemo mfumo wa kutoa taarifa za rushwa (Takukuru kupitia namba 113), mfumo wa taarifa na shughuli za bunge, mfumo wa ajira unaorahisisha mchakato wa ajira za serikalini na mfumo wa malipo ya serikali kielekroni (GePG) unaowezesha udhibiti wa ukusanyaji wa maduhuli kielekroni serikalini.


Amesema wamejizatiti vyema kuanza kipindi kingine cha miaka mitano ya utekelezaji kuanzia 2016/2017 hadi 2020/2021  ili kufanya matumizi ya Tehama yawe na manufaa zaidi katika utendaji  wa taasisi za umma.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search