Waliotaka kusafirisha madini bilioni 1.5 wapandishwa kizimbani...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abdulrahim Sadiki
MFANYABIASHARA Naushad Mohammed Suleiman (63) na Ali Makame (36) wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa  kusafirisha madini ya dhahabu vipande saba vyenye thamani ya bilioni 1.5 bila ya kuwa na leseni


Wamesomewa makosa yao leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri na Wakili wa serikali, Jehovanes Zacharia.

Wakili Zacharia  amedai  washtakiwa hao wanakabiliwa na makosa mawili  ikiwemo la uhujumu uchumi.

Wakili Zacharia amedai katika shtaka  la kwanza la kula njama kuwa  washtakiwa hao walitenda shtaka hilo  tarehe tofauti kati ya Novemba mosi na 29, 2017.
Amedai  katika tarehe hizo washtakiwa hao wakiwa maeneo ya Geita Mjini na Dar es Salaam walikula njama na watu wengine ambao hawakufikishwa mahakamani ili wasafirishe madini ya dhahabu nje ya nchi bila ya kuwa na Leseni.

Pia wanadaiwa  kusafirisha madini bila ya kuwa na kibali, inadaiwa kuwa  walitenda shtaka hilo Novemba 29,2017 katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman Karume Zanzibar.

Ambapo  walikutwa wakisafirisha madini ya dhahabu vipande saba vikiwa na uzito wa Kilo.18.354 yakiwa na thamani ya Sh 1,505,009,929.38.

Baada ya kusomewa mashtaka yao, Hakimu Mashauri amesema washtakiwa hawatakiwi kujibu kitu chochote kwa sababu Mahakama hiyo haina mamlaka ya kuisikiliza kesi hiyo hadi Mahakama Kuu.


Wakili Zacharia amedai  kuwa upelelezi wa kesi hiyo namba 81 ya mwaka 2017 bado haujakamilika  na kesi imeahirishwa hadi
Desemba 20,2017.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search