Wanawake waliovaa suruali wakamatwa...soma habari kamili na matukio360...#share


Na mashirika ya kimataifa
WANAWAKE 24 wa Sudan wameshtakiwa kwa kujivunjia heshima, baada ya kuonekana wamevaa suruali katika karamu moja mjini Khartoum.

Baadhi ya wanawake wakiwa wamevaa suruali

Karamu hiyo ilivamiwa na polisi wa nidhamu  wiki iliyopita.

Suruali zinachukuliwa na wakuu kuwa vazi la utovu wa adabu, na adhabu yake ni mijeledi 40 pamoja na faini.

Wanaharakati wanasema maelfu ya wanawake wanakamatwa kila mwaka, na kuchapwa mijeledi.

Wanasema sheria inayopiga marufuku suruali na sketi fupi na za kubana, inawabagua wakristo, na inatumiwa kiholela. Kawaida wanaweke nchini Sudan huvaa nguo ndefu.

Katika suala la mavazi kila nchi inauamuzi wake nchini Austaria mavazi ya niqab na burka yamepigwa marufuku



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search