ACT Wazalendo watoa neno uchaguzi Kinondoni, Siha...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

WAKATI chama cha Chadema kikibadilisha msimamo wake, chama cha ACT-Wazalendo kimeendelea na msimamo wake wa kutoshiriki kwenye uchaguzi mdogo wa ubunge katika jimbo la Siha na Kinondoni, utakaofanyika Februari 17,2018 
Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe.

Hivi karibuni Chadema ilitangaza wagombea katika majimbo hayo ikiashiria kutengua msimamo ambao walikuwa nao awali wa kususia uchaguzi mdogo wa marudio hadi hapo  NEC itakapokutana na wadau wa vyama vya kujadili na kuondoa dosari mbalimbali.

Akizungumza jijini Dar es Salaam na matukio360, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa ACT-Wazalendo Addo Shaibu amesema hawatashiriki hadi hapo dosari zilizojitokeza katika uchaguzi mdogo wa udiwani zitakapokuwa zimeshughulikiwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

“Sisi msimamo wetu uko pale pale kwamba  kuna mapungufu makubwa sana ya kidemokrasia yanayo tokea katika michakato hii ya uchaguzi ambayo yanapaswa kushughulikiwa ndio maana utaona tumechukua jitihada kubwa kuwafikia wenzetu, ili kupanga  mkakati wa pamoja wa kuona jinsi ya kuyarekebisha,” amesema Shaibu.

Shaibu amesema tangu dosari zilipotokea na kupeleka malalamiko NEC ili zishughulikiwe, kwa mujibu wa tathmini yao inaonesha kwamba matatizo mengi hayajashughulikiwa.

Ameongeza kuwa baada ya vyama vya upinzani kutangaza  kususia uchaguzi NEC ilifanyia kazi suala moja tu miongoni mwa mengi yaliyolalamikia suala hilo ni wakuu wa wilaya kuingilia uchaguzi.

Hivyo NEC katika jambo hilo ilichukua hatua kwa kuwaandikia wakuu wa wilaya barua ikiwataka kutojihusisha na masuala ya uchaguzi.

Amesema hilo ni jambo dogo kwani hadi sasa hawajashughulikia suala la vyombo vya dola kuingilia uchaguzi kwa kuvitisha na kamata kamata dhidi ya viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani.

“Hilo ni suala dogo kuna kamata kamata, matumizi ya nguvu ya kutumia vyombo vya dola hasa polisi na jinsi na uongo katika utangazaji wa wa matokeo,” amesema.
Amesema kuna umuhimu wa kuendelea kushinikiza ili mchakato wa uchaguzi uwe huru na haki.

“Kwa hiyo sasi tunaendelea kuweka shinikizo na hatutoshiriki kwenye uchaguzi huu wa kinondoni na Siha hadi pale ambapo angalau tume itakaposhughulikia malalamiko yetu,” ameongeza.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search