Akamatwa na dawa za kulevya uwanja wa ndege...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Salha Mohamed, Dar es Salaam
JESHI la Polisi Kikosi cha Viwanja vya Ndege jijini Dar es Salaam, linamshikilia raia wa Nigeria, Christian Ugbechi(26) akiwa na pipà 59 zenye zaidi ya gram 800 za dawa za kulevya aina ya Cocaine.
Akizungumza na matukio360 kamanda wa Viwanja vya Ndege, Matanga Mbushi amesema Januari 29 majira ya 8:15 mchana eneo la ukaguzi abiria wa nje uwanjani hapo walimtilia shaka abiria huyo.
"Mnigeria huyo anaishi na kufanya kazi nchini ufaransa alikuwa akisafiri na ndege ya Shirika la ndege la Ethiopia kuelekea Ufaransa kupitia Adis Ababa Ethiopia,"amesema.
Amesema pipi 56 amezificha ndani ya boksi alilokuwa amebeba mgongoni huku tatu akiwa amemeza tumboni.
"Bado yupo chini ya uangalizi maalum wa Polisi kuhakikisha anazitoa pipi zote alizomeza tumboni,"amesema.
Amefafanua kuwa jeshi la Polisi linatoa onyo kali kwa mtu mwenye nia ovu kupitia viwanja vya ndege kusafirisha dawa za kulevya kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
JESHI la Polisi Kikosi cha Viwanja vya Ndege jijini Dar es Salaam, linamshikilia raia wa Nigeria, Christian Ugbechi(26) akiwa na pipà 59 zenye zaidi ya gram 800 za dawa za kulevya aina ya Cocaine.
Akizungumza na matukio360 kamanda wa Viwanja vya Ndege, Matanga Mbushi amesema Januari 29 majira ya 8:15 mchana eneo la ukaguzi abiria wa nje uwanjani hapo walimtilia shaka abiria huyo.
"Mnigeria huyo anaishi na kufanya kazi nchini ufaransa alikuwa akisafiri na ndege ya Shirika la ndege la Ethiopia kuelekea Ufaransa kupitia Adis Ababa Ethiopia,"amesema.
Amesema pipi 56 amezificha ndani ya boksi alilokuwa amebeba mgongoni huku tatu akiwa amemeza tumboni.
"Bado yupo chini ya uangalizi maalum wa Polisi kuhakikisha anazitoa pipi zote alizomeza tumboni,"amesema.
Amefafanua kuwa jeshi la Polisi linatoa onyo kali kwa mtu mwenye nia ovu kupitia viwanja vya ndege kusafirisha dawa za kulevya kwamba hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
No comments:
Post a Comment