Shughuli za kiuchumi, kijamii zaathiri mazingira nchini...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

SERIKALI imesema kasi ya ukuaji wa uchumi na kupanuka kwa shughuli za kijamii inasababisha kuongezeka kwa changamoto za masuala ya uhifadhi wa mazingira na usimamizi sahihi na endelevu kwa rasilimali nchini.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Profesa Faustine Kamuzora alipokuwa akizindua warsha ya wadau kuhusu upatikanaji wa takwimu za kupima na kutathmini utekelezaji wa mpango wa pili wa maendeleo wa taifa wa miaka mitano na viashiria vya malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) katika sekta ya mazingira na matumizi endelevu ya rasilimali.

Kutokana na changamoto hiyo, Prof. Kamuzora amesema serikali imefanya jitihada kuweka mfumo wa kisheria na kitaasisi ili kudhibiti huhifadhi wa mazingira ikiwa ni pamoja na kuingiza masuala hayo kwenye sera ya mipango ya maendeleo kitaifa.

“Kutokana na changamoto zinazosababishwa na kasi ya ukuaji wa uchumi na kupanuka kwa shughuli za kijamii serikali imefanya jitihada kubwa katika kuweka mfumo wa kisheria na kitaasisi katika kudhibiti masuala ya uhifadhi wa mazingira ikiwa ni pamoja na kuingiza masuala ya mazingira kwenye sera ya mipango ya maendeleo ya kitaifa,” amesema Prof. Kamuzora

Ameongeza “ kunajitihada mbali mbali kama mnavyofahamu, kuna sera yazamani kidogo ya 1997 ambayo kwa sasa imehuishwa kuwa ya mazingira na  kunasheria ya mazingira ya mwaka 2004 yenyewe ishafanyiwa marekebisho kidogo."

Akizungumzia warsha hiyo, amesema kuwa anaamini wadau hao watakuja na jibu la jinsi ya kutumia mazingira na rasilimali vizuri kwa ajili ya maendeleo endelevu.

Prof. Kamuzora ameongeza kuwa katika mpango wa maendeleo wa miaka mitano masuala ya mazingira yamewekwa ili kuhakikisha mazingira hayaathiriwi kwa namna yoyote ile.


Ameeleza kuwa  Ofisi ya Takwimu (NBS) kwa kushurikiana na wadau mbali mbali wameunda kamati tendaji ambayo inahusisha sekta binafsi, umma na asasi za kiraia kuhakikisha kwamba hakuna mtu anayeachwa nyuma katika suala la uhifadhi wa mazingra.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search