BoT yazifunga benki tano....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT)  imezifunga, kusitisha shughuli zote za kibenki, kufuta leseni za kibiashara ya kibenki, benki tano na kuziweka chini ya ufilisi kuanzia leo kutokana na kutotimiza matakwa ya kisheria ya kuwa na mtaji kamili na wakutosha.
Profesa Benno Ndulu.

Pia benki tatu kati ya nane, Kilimanjaro Coorperative Bank Limited, Tanzania Women’s Bank Plc, na Tandahimba Community Bank Limited zimepewa muda wa miezi sita hadi Juni 30, 2018 kuweka kiwango cha mtaji kinachokidhi matakwa ya kisheria na kizishindwa zitafungwa.

Uamuzi huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Gavana wa BoT Profesa Benno Nduru alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.

“Banki zinazochukuliwa hatua hii Covenant Bank for Women (Tanzania) Limited, Efatha Bank Limited, Njombe Community Bank Limited, Kagera Farmers’ Coorperative Bank Limited na Meru Community Bank Limited,” amesema Profesa Ndulu.

Amesema uamuzi huo umefikiwa kwa mujibu wa kifungu cha 56 (1) (g), 56 (2) (a), (b) na (d), 58 (2) (i), 11 (3) (c) na (j), 61 (1) na 41 (a)cha sheria ya mabenki  na taasisi za fedha ya mwaka 2016.


Ameuhakikishia umma kuwa BoT itaendelea kulinda maslahi ya wenye amana katika mabenki kwa lengo la kuleta uhimilivu katika sekta ya fedha.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search