Waziri Jafo ampa mkurugenzi Ilala siku saba...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Salha Mohamed,Dar es Salaam
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI),suleiman Jafo ametoa siku saba kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Msongela Palella kuhakikisha anakarabati barabara ya Buguruni Mnyamani jijini Dar es Salaam.
Amesema endapo barabara hiyo haitakarabatiwa hataweza kuvumilia na kwamba atawafukuza watumishi wazembe huku akimtaka Mkurugenzi kuwasiliana na Mamlaka ya Maji safi na maji taka (DAWASCO) kudhibiti mabomba yaliyopasuka.
"Kama mkiamua kuifunga hii barabara sawa... Lakini nikipita nikakuta kazi haijaanza mtaniona mbaya.
"Watu wanapoteza maisha, nikute watu wanafanya kazi... Nawapa 'Black and white' nikikuta uzembe nitaondoka na mtu hapa,"amesema.
Akizungumzia utupaji taka jirani na hospitali ya Mnyamani, Jafo amepiga marufuku kutupa taka eneo hilo na kuagiza kufanyiwa maboresho hospitali hiyo.
Mkurugenzi wa Ilala, Palella amesema atatekeleza agizo hilo na kwamba wapo kwenye mchakato wa kuboresha hospitali hiyo.
"Tumeshatenga fedha za fidia kwa kaya 9 sh milioni 489 ili kupisha uboreshaji wa hospitali... Leo tutakaa na Dawasco kupanga mpango kazi ili kuanza kukarabati barabara, "amesema.
Mbunge wa Segerea, Bonnah Kaluwa amesema ameshafanya ziara eneo hilo mara kumi hivyo amempongeza waziri Jafo kufika na kuchukua hatua.
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI),suleiman Jafo ametoa siku saba kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala, Msongela Palella kuhakikisha anakarabati barabara ya Buguruni Mnyamani jijini Dar es Salaam.
Amesema endapo barabara hiyo haitakarabatiwa hataweza kuvumilia na kwamba atawafukuza watumishi wazembe huku akimtaka Mkurugenzi kuwasiliana na Mamlaka ya Maji safi na maji taka (DAWASCO) kudhibiti mabomba yaliyopasuka.
"Kama mkiamua kuifunga hii barabara sawa... Lakini nikipita nikakuta kazi haijaanza mtaniona mbaya.
"Watu wanapoteza maisha, nikute watu wanafanya kazi... Nawapa 'Black and white' nikikuta uzembe nitaondoka na mtu hapa,"amesema.
Akizungumzia utupaji taka jirani na hospitali ya Mnyamani, Jafo amepiga marufuku kutupa taka eneo hilo na kuagiza kufanyiwa maboresho hospitali hiyo.
Mkurugenzi wa Ilala, Palella amesema atatekeleza agizo hilo na kwamba wapo kwenye mchakato wa kuboresha hospitali hiyo.
"Tumeshatenga fedha za fidia kwa kaya 9 sh milioni 489 ili kupisha uboreshaji wa hospitali... Leo tutakaa na Dawasco kupanga mpango kazi ili kuanza kukarabati barabara, "amesema.
Mbunge wa Segerea, Bonnah Kaluwa amesema ameshafanya ziara eneo hilo mara kumi hivyo amempongeza waziri Jafo kufika na kuchukua hatua.
No comments:
Post a Comment