Dawa za kuongeza nguvu za kiume zazua balaa....soma habari kamili na matukio 360...#share
Na mashirika ya kimataifa
WANAUME watatu nchini Zambia wamelazwa kwa makosa katika wadi ya wagonjwa wa kipindupindu baada ya kunywa dawa za asili zinazodaiwa kuongeza nguvu za kiume.
Wanaume hao watatu wanatoka katika mji mdogo wa katete, na si wagonjwa wa kipindupindu bali walikunywa dawa ya kuongeza nguvu ya kufanya tendo la ndoa inayojulikana kama Mvubwe.
Watu waliokunywa dawa za kuongeza nguvu za kiume wakiwa wamelazwa wakipatiwa matibabu
Kiongozi wa mkoa, Chanda Kasolo amesemaa mara baada ya kunywa dawa hizo, walianza kutapika kitu ambacho kilisababishwa na mchanganyiko wa chakula, pombe na dawa hizo za asili.
''Baada ya majibu ya vipimo kupatikana , inaonekana kuwa mchanganyiko wa pombe, vyakula na dawa hiyo, ulisababisha mchafuko wa mfumo wa chakula na hivyo ikahusishwa na kipindupindu lakini baada ya kuwauliza maswali, baadaye walikiri kuwa walikunywa dawa ya kuongeza nguvu katika tendo la ndoa''
Wagonjwa hao bado wapo katika kituo hicho cha kipindupindu na wanaendelea vizuri na matibabu, aliongeza Kasolo.
Ugonjwa wa kipindupindu uliolipuka mwaka jana ulisababisha vifo vya watu takribani 70, kusini mwa Afrika.
Rais Edgar Lungu mwezi uliopita, alitoa agizo kwa jeshi la Zambia kusafisha maeneo ya masoko na kuondoa uchafu ambao ndio sababu ya kipindupindu.
No comments:
Post a Comment