Donald Trump, Kim Jon-un watunishiana misuli....soma habari kamili na matukio360...#share

Na mashirika ya kimataifa
Rais wa Marekani, Donald Trump amejigamba kuwa kibonyezo chake cha silaha za nyuklia ni kikubwa na kilicho na nguvu zaidi kuliko kile cha kiongozi wa Korea Kaskazini,Kim Jon-un.
Rais wa Marekani, Donald Trump
Trump amejibu mapigo hayo  kupitia akaunti yake ya  Twitter ikiwa ni  majibizano kati ya viongozi wa mataifa hayo mawili yaliyo na silaha za nyuklia.
Mapema wiki hii katika salam zake za mwaka mpya 2018,Kim alionya kuwa kibonyezo chake cha nyuklia kipo kwenye meza yake.
Korea Kaskazini inadai kuwa ina silaha za nyuklia na inaweza kuishambulia Marekani huku wadadisi wakisema kuwa ikiwa Korea Kaskazini ina silaha za nyuklia, je ina teknolojia ya kuzitumia?.
Kando na kuitishia Marekani, ujumbe wa mwaka mpya wa Kim pia uliwashangaza wengi wakati alisema kuwa alikuwa tayari kwa mazungumzo na Korea Kusini na angependa kuituma timu kwa mashindano ya olimpiki ya msimu wa baridi nchini Korea Kusini mwezi ujao.

Tayari mapema hii leo mawasiliano ya simu baina ya Korea Kusini na Kaskazini yamerejea. Tangu mwaka 2016 Korea Kaskazini ilikata uhusiano huo

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search