Kambi ya upinzani yasusa Bungeni....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

WIZARA ya Katiba na Sheria kambi rasmi ya upinzani bungeni imesusa kusoma maoni ya upinzani kuhusu mswada wa marekebisho ya sheria mbali mbali nchini.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kumzuia Ally Salehe kusomwa kwa baadhi ya maneno yaliyomo katika maoni hayo.

Salehe alikuwa akisoma maoni hayo leo kwa niaba ya Msemaji wa Wizara hiyo Tundu Lissu aliyeko nchini Ubelgiji kwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi Novemba 7 mwaka jana.

Maneno yaliyozuiwa kusomwa na upinzani ni kuhusu matukio ya uhalifu nchini, likiwemo la kushambuliwa kwa Mbunge wa Singida Mashariki na Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Tundu Lissu.

Salehe alianza kusoma maneno hayo lakini alipofika aya ya nne alizuiwa na Chenge akimtaka asubiri ambapo baadae alimueleza kuwa lugha iliyotumika katika ukurasa wa kwanza na wa pili wa hotuba hiyo si ya kibunge.

Baada ya kauli hiyo, Salehe amesema upinzani unaiamini na unaisimamia hotuba hiyo kwa kuwa wabunge wote wanayo nakala yake na kuomba kuiwasilisha na kurejea kuketi.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search