UPDATES: Tundu Lissu aondoka kwenda Ubelgiji....soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu
MWANASHERIA mkuu wa chama cha Chadema, Tundu Lissu mapema asubuhi ya leo ameondoka kwenda nchini Ubelgiji kwa matibabu ya viungo.
Tundu Lissu akitoka hospitali jijini Nairobi Kenya kuelekea uwanja wa ndege tayari kwa safari ya kwenda nchini Ubelgiji
Jioni Jana akizungumza na matukio360, Lissu alisema fedha za matibabu zinagharamiwa na wadau wa vyama vya upinzani na marafiki mbalimbali.
"Nashukuru Mungu inaendelea vizuri lakini ninakwenda Ubelgiji kwa matibabu ya viungo kwani mtu ilikata muda mrefu unapoteza uwezo wako wa kawaida wa kutembea. Fedha za matibabu zinagharamiwa na wadau wa vyama vya upinzani na marafiki mbalimbali," alisema
Septemba 7, 2017 Lissu ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashirika alipigwa risasi mjini Dodoma alipokuwa anahudhuria vikao vya Bunge la Tanzania. Amelazwa katika hospitali mjini Nairobi kwa takribani miezi minne.
MWANASHERIA mkuu wa chama cha Chadema, Tundu Lissu mapema asubuhi ya leo ameondoka kwenda nchini Ubelgiji kwa matibabu ya viungo.
Tundu Lissu akitoka hospitali jijini Nairobi Kenya kuelekea uwanja wa ndege tayari kwa safari ya kwenda nchini Ubelgiji
Jioni Jana akizungumza na matukio360, Lissu alisema fedha za matibabu zinagharamiwa na wadau wa vyama vya upinzani na marafiki mbalimbali.
"Nashukuru Mungu inaendelea vizuri lakini ninakwenda Ubelgiji kwa matibabu ya viungo kwani mtu ilikata muda mrefu unapoteza uwezo wako wa kawaida wa kutembea. Fedha za matibabu zinagharamiwa na wadau wa vyama vya upinzani na marafiki mbalimbali," alisema
Septemba 7, 2017 Lissu ambaye pia ni mbunge wa Singida Mashirika alipigwa risasi mjini Dodoma alipokuwa anahudhuria vikao vya Bunge la Tanzania. Amelazwa katika hospitali mjini Nairobi kwa takribani miezi minne.




No comments:
Post a Comment