UPDATES: Tundu Lissu atoka hospitali kwenda Ulaya...soma habari kamili na matukio360..#share
Na mwandishi wetu
MWANASHERIA mkuu wa chama cha Chadema, Tundu Lissu ameruhusiwa kutoka hospitali nchini Kenya na kesho anasafiri kwenda barani Ulaya kwa matibabu ya viungo.
Tundu Lissu
Akizungumza na matukio360 Kwa njia ya simu jioni hii, Lissu amesema mapema kesho asubuhi anasafiri kwenda Ulaya.
"Siwezi kusema ni nchi gani barani Ulaya ninayokwenda kwa sababu za kiusalama. Afya yangu imetengemaa ninakwenda kwa ajili ya matibabu ya viungo," amesema Lissu
Lissu ametibiwa kwa takribani miezi minne nchini Kenya baada ya kupigwa risasi mjini Dodoma Septemba 7, 2017
MWANASHERIA mkuu wa chama cha Chadema, Tundu Lissu ameruhusiwa kutoka hospitali nchini Kenya na kesho anasafiri kwenda barani Ulaya kwa matibabu ya viungo.
Tundu Lissu
Akizungumza na matukio360 Kwa njia ya simu jioni hii, Lissu amesema mapema kesho asubuhi anasafiri kwenda Ulaya.
"Siwezi kusema ni nchi gani barani Ulaya ninayokwenda kwa sababu za kiusalama. Afya yangu imetengemaa ninakwenda kwa ajili ya matibabu ya viungo," amesema Lissu
Lissu ametibiwa kwa takribani miezi minne nchini Kenya baada ya kupigwa risasi mjini Dodoma Septemba 7, 2017
No comments:
Post a Comment