Vigogo Six Telecoms waendelea kusota rumande...soma habari kamili na matukio 360..#share

Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

KESI ya uhujumu uchumi inayowakaili vigogo wa kampuni ya mawasiliano ya Six Telecoms, akiwemo wakili Dk. Ringo Tenga na wanzake imeahirishwa hadi Januari 26, 2018 kutokana na upelelezi kutokamilika.
Pichani ni Watuhumiwa wa kesi ya uhujumu uchumi inayowakabili vigogo hao Watatu wa Kampuni ya mawasiliano ya Six Telecoms, akiwemo Wakili Dk Ringo Tenga na wenzake wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu .

Mbali na Dk. Tenga, washitakiwa wengine ni Mfanyabiashara Peter Noni, Mhandisi na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni hiyo, Hafidhi Shamte, Mkuu wa fedha wa kampuni hiyo, Noel Odeny Chacha na Kampuni ya Six Telecoms Limited.

Wakili wa Serikali, Leonard Challo alidai mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Victoria Nongwa kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi bado unaendelea.

Hakimu Nongwa aliahirisha kesi hiyo hadi Januari 26, mwaka huu kwa ajili ya kutajwa.

Katika kesi hiyo namba 73 ya 2017, inadaiwa kati ya Januari 1, 2014 na Januari 14,2016 Dar es Salaam washitakiwa, walitoza malipo ya simu za kimataifa kwa kiwango cha dola 0.25 kwa dakika kwa lengo la kujipatia faida.

Pia washtakiwa hao wanadaiwa katika tarehe hizo, washtakiwa waliisababishia TCRA hasara ya Dola za Marekani 3,736,861, sawa na Sh bilioni nane.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search