Vigogo watatu Maliasili wapandishwa kizimbani ....soma habari kamili na matukio 360...#share

Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam
WAFANYAKAZI watatu wa Wizara ya Maliasili na Utalii  leo wamepandishwa kizimbani katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu kwa tuhuma za kuisababishia serikali hasara ya dola 32,599.


Wakili wa Serikali kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini(Takukuru) Leonard Swai, amewataja washtakiwa hao ni, Ofisa Muhifadhi anayehusika na uwindaji wa matumizi endelevu ya wanyamapori Rajabu Hochi, Ofisa wa Muhifadhi mwenye wajibu wa kukusanya wa mapato ya uwindaji , Mohamed Madehele na Isaac Maji.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri imedaiwa kuwa, washtakiwa wakiwa watumishi kitengo cha Wanyamapori, walitenda makosa hayo katika makao makuu ya wizara hiyo.

Akisoma hati ya mashtaka wakili wa serikali Pendo Temu amedai,kati ya Januari 12 na Desemba 31, mwaka 2008, makao makuu ya wizara hiyo, Hochi na Madehele wakiwa watumishi wa wizara hiyo, wakiwa na wajibu wa kukusanya mapato yanayotokana na uwindaji walitumia madaraka yao vibaya kwa kuzidisha wanyama pori kwa Kampuni ya Uwindaji ya Northern Hunting Enterprises (Tanzania) kinyume cha sheria na hivyo kuiwezesha kampuni hiyo kupata faida ya USD 250 isivyo halali.

Pia Hochi na Madehele, wanadaiwa kati ya Agosti 11 na Desemba 31, mwaka 2011, makao makuu ya wizara hiyo,waliiwezesha kampuni hiyo kujipatia dola za Marekani 250 isivyo halali.Aidha, Hochi na Madehele, wanadaiwa, kati ya Septemba 5 na Desemba 31,mwaka 2010, walishindwa kukusanya faini ya dola za Marekani 15,630 kutoka katika kampuni hiyo.

Washtakiwa Hochi na Madehele,wanadaiwa kushindwa kukusanya faini ya dola za Marekani 250 kutoka kampuni ya uwindaji ya Hunting Enterprises (Tanzania), kinyume cha sheria.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search