Weah kuapishwa leo Wenger, Drogba, Etoo kushuhudia...soma habari kamili na matukio360...#share
Na mashirika ya kimataifa
RAIA wa Liberia wamekesha kuamkia leo katika uwanja mkuu wa taifa katika jiji la Monrovia kusheherekea uapishwaji wa rais mteule wa nchi hiyo, George Weah huku kocha Aserne Wenger, mchezaji Samuel Etoo na Didier Drogba ni miongoni mwa watakaoshuhudia kuapishwa kwake.
Weah aliyeshinda duru mbili za uchaguzi anaapishwa rasmi leo kuchukua nafasi ya mtangulizi wake, Ellen Jonson Sirleaf ambaye alikuwa rais wa kwanza mwanamke nchini humo.
Rais mteule wa Liberia, George Weah
Weah ambaye ni Mwafrika wa kwanza kuchukua tuzo ya mchezaji bora wa Dunia wa shirikisho la soka Duniani(FIFA) alimshinda makamo wa rais wa nchi hiyo, Joseph Boakai.
RAIA wa Liberia wamekesha kuamkia leo katika uwanja mkuu wa taifa katika jiji la Monrovia kusheherekea uapishwaji wa rais mteule wa nchi hiyo, George Weah huku kocha Aserne Wenger, mchezaji Samuel Etoo na Didier Drogba ni miongoni mwa watakaoshuhudia kuapishwa kwake.
Weah aliyeshinda duru mbili za uchaguzi anaapishwa rasmi leo kuchukua nafasi ya mtangulizi wake, Ellen Jonson Sirleaf ambaye alikuwa rais wa kwanza mwanamke nchini humo.
Rais mteule wa Liberia, George Weah
Weah ambaye ni Mwafrika wa kwanza kuchukua tuzo ya mchezaji bora wa Dunia wa shirikisho la soka Duniani(FIFA) alimshinda makamo wa rais wa nchi hiyo, Joseph Boakai.
Alishinda katika uchaguzi baada ya kushinda katika wilaya 12 miongoni mwa 15 zilizomo katika nchi hiyo ya Afrika ya Magharibi.
Weah ametuma ujumbe katika mtandao wa Twitter kuwashukuru watu wote waliompigia kura akisema mipango yake ni kuleta ukombozi kwa nchi nzima.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu ya AC Milan ya Italia, anakuwa rais wa 25 wa nchi hiyo ambapo aliyekuwa makamu wa rais kwa miaka 12 iliyopita, Joseph Boakai, alipata ushindi katika wilaya mbili tu.
No comments:
Post a Comment