BoT yapiga 'stop' maduka 86 ya kubadilishia fedha...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Mtwara
BENKI Kuu ya Tanzania  (BoT) imeyafutia leseni maduka 86 ya kubadilishia fedha za kigeni baada ya kushindwa kutimiza masharti.

Masharti hayo ni paomoja na kushindwa  kutoa vielelezo vinavyoonyesha vyanzo vya fedha hizo zinazotumika kwenye biashara hiyo.
Akizungumza leo na waandishi wa habari waliohudhuria mafunzo ya kuandika habari za kiuchmi mkoani Mtwara meneja wa kitengo kinachosimamia fedha za kigeni kutoka BoT Eliyamringi Mandari amesema kufungwa kwa maduka hayo kunatokana na oparesheni inayoendelea nchi nzima kwa sasa yenye lengo la kuleta ufanisi wa kazi katika maduka hayo.
“Opereresheni hii inakwenda sambamba na usajili mpya wa maduka haya ya kubadilisha fedha za kigeni ambayo umetokana na kanuni mpya ya kuyasimamia, lengo hasa ni kuongeza ufanisi na  mitaji katika kuendesha biashara hii,” amesema Mandari.
Hata hivyo amesema katika oparasheni hiyo maduka 297 yametuma maombi ya kupatiwa leseni huku 65 yakiendelea kufanyiwa kazi na 71 tayari yamepatiwa leseni mpya pamoja na matawi yake arobaini.
Mandari amesisitiza kuwa baada ya wiki mbili zijazo zoezi hilo litakuwa limilika na taarifa kamili itatolewa.
Ameeleza kwamba ni kosa la jinai kwa mtu yeyote kuendesha biashara ya fedha za kigeni bila leseni ya benki kuu na adhabu yake ni faini ya sh. milioni 4 ama kifungo cha miaka 14 gerezani au vyote viwili kwa pamoja.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search