Waziri ateketeza eka sita za bangi ...soma habari kamili na matukio360...#share
Na
Mwandishi Wetu, Arusha
WAZIRI wa
mambo ya ndani nchini, Dkt Mwigulu Nchemba leo ameongoza oparesheni ya
kuteketeza jumla ya ekari sita za bangi zilizokuwa zimelimwa katikati ya msitu ndani ya kijiji cha Engalaoni wilayani Arumeru mkoani Arusha.
Waziri wa mambo ya ndani nchini, Dk. Mwigulu Nchemba leo
ameongoza oparesheni ya kuteketeza jumla ya ekari sita za bangi
zilizokuwa zimelimwa katikati ya msitu ndani ya kijiji cha Engalaoni
wilayani Arumeru mkoani Arusha.
Dk. Nchemba akishirikiana na kamanda wa jeshi la polisi mkoani Arusha,(RPC) Charles Mkumbo pamoja na vikosi vya askari wa jeshi la polisi
mkoani hapa walilazimika kuacha magari yao njiani na kutembea umbali wa kilomita 5 milimani kufika katikati ya msitu huo ambapo wamiliki
wa mashamba hayo walitokomea kusikojulikana.
Akizungumza
na waandishi wa habari wakati wa zoezi hilo Mwigulu alisema kwamba serikali
itaendelea na oparesheni pande zote za nchi na haitasita kuwakamata
wahusika wote na kutaifisha magari yatakayotumika kusafirisha bangi.
Mbali na
kuwapongeza askari walioshiriki katika zoezi hilo kwa kazi nzuri
wanayofanya ya kuteketeza dawa za
kulevya shambani, amewataka waongeze juhudi pia katika kupambana na madawa
ya kulevya yanayotengenezwa viwandani.
No comments:
Post a Comment