CCM yashinda Siha....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Kilimanjaro

MGOMBEA ubunge kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mdogo wa marudio jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro Dk. Godwin Molel ametangazwa kuwa mshindi.





Dk. Godwin Molel akikabidhiwa cheti cha ushindi wa ubunge jimbo la Siha

Akitangaza matokeo msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo Valerian Juwal, amesema kuwa Dk. Molel amepata kura 25611 akifuatiwa na mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Elvis Mosi aliyepata kura 5905.


Mgombea wa Chama cha Wananchi CUF Tumsifuel Mwanri amepata kura 274 huku wa Chama cha SAU Azaria yeye akipata kura 170.

Uchaguzi wa marudio wa jimbo hilo ulifanyika jana sambamba na jimbo la Kinondoni na kata nane.



Ccm            25,611 sawa na 80%.
Chadema 5,905     sawa na 18.5%.
CUF         274        sawa na 0.9%.

SAU         170       sawa na 0.6%.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search