Chadema walituhumu jeshi la polisi..... soma habari kamili na matukio360...#share
Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
CHAMA cha Chadema kimelituhumu Jeshi la Polisi, ikidai jeshi hilo lililenga kuwashambulia kwa risasi viongozi wa chama hicho.
Kulia ni Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na
Mambo ya Nje wa Chadema John Mrema, Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo Banson Kigaila na Ofisa Habara wa Chadema Tumain Makene wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo.
Pia kimemtaka Waziri wa
Mambo ya Ndani ya Nchi Dk. Mwigulu Nchemba na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP)
Simon Sirro wajiuzulu kutokana na shambulio hilo.
Shutuma hiyo imetolewa
leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo wa Chadema
Benson Kigaila alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari na kudai jeshi hilo limejeruhi raia na kusababisha kifo cha mwanafunzi wa chuo cha NIT walipokuwa wakiandamana
kuelekea kwa mkurugenzi wa Kinondoni.
“Tunasema shambulizi
hili la risasi lilikuwa linawalenga viongozi wetu, ukiacha mwanafunzi Akwilina
Akwilini aliyefariki kwa kupigwa risasi, wengine waliojeruhiwa ni walinzi
wa viongozi wetu, kwa hiyo lazima tusema kwamba walikuwa wanalenga viongozi,”
amesema Kigaila.
Amesema walinzi hao
walishambuliwa sehemu za nyonga na mapajani na kuwataja kuwa
ni Erick John aliyepigwa risasi katika paja la mguu wa kulia na amelazwa katika
hospitali ya Mwananyamala.
Wengine ni Innocent
Mushi aliyejeruhiwa kwenye nyonga na kupelekwa hospitali ya Mwananyama kupewa rufaa ya kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) yupo
hadi sasa, na Rukia ambaye alipelekwa Mwananyamala lakini ndugu zake walimhamisha.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa chama
hicho John Mrema amesema jeshi kushambulia raia, kuwajeruhi na
kuua wasilichukulie kama ni suala dogo.
“Tunataka
serikali ichukue hatua kwa wale wote waliohusika na mauaji haya, hatujui hadi
sasa Mwigulu na IGP wapo ofisini, kama kweli wameguswa na mauaji haya wajiuzulu,”
amesema Mrema.
Katika
hatua nyingine wameshangaa kauli ya Katibu wa Itikani na Uenezi wa Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole ya kudai kuwa waliosababisha mauaji hayo ni
Chadema kwa kufanya maandamano na kulitaka Jeshi la Polisi kumkamata mwenyekiti
wa chama hicho Freeman Mbowe na kumchukulia hatua.
Mrama
amedai kauli hiyo imewashtua na ni ya ajabu na si ya
kiuongozi.
“Tunaliomba
jeshi la polisi likamhoji Polepole huenda analijua vizuri tukio hili, lakini
niwaambie CCM suala hili la kuteka
kuuawa halitaishia kwa Chadema bali litaenda hadi kwa wana CCM,” amesema
Mrema.
No comments:
Post a Comment