Polisi sita washikiliwa mauaji mwanafunzi NIT....soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Dar es salaam
KUFUATIA tukio la kupigwa risasi kwa mwanafunzi Akwilina Akwilini, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema jeshi hilo linawashikilia askari polisi sita waliotumia silaha za moto kuwadhibiti waandamanaji katika Jimbo la Kinondoni.
Pia linawashikiria watu 40 kwa mahojiano kuhusiana na tukio hilo.
Pia linawashikiria watu 40 kwa mahojiano kuhusiana na tukio hilo.
Lazaro Mambosasa
Amesema silaha za askari hao zimedhibitiwa kwa uchunguzi na kwamba hatua za kisheria zitachuliwa dhidi ya waliohusika na kifo hicho.
Kifo hicho kilifuatia baada ya kuibuka makabiliano kati ya jeshi la polisi na wafuasi wa chama cha Chadema
Walioshuhudia wanasema kuwa maafisa wa polisi walitumia vitoa machozi na risasi katika harakati za kuwatawanya mamia ya wafuasi wa chama cha Chadema waliokuwa wakiandamana hadi afisi za tume ya uchaguzi.
Baadhi ya wanachama wa chama hicho walikamatwa.Mwili wa msichana huyo ulikuwa na jeraha la risasi kichwani
Kwa mujibu wa uongozi wa chuo hicho, mwanafunzi huyo alikuwa safarini kulekea Bagamoyo kupeleka fomu za kuomba nafasi ya kufanya mafunzo kwa vitendo mjini Bagamoyo.
About Author Matukio360
Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.
No comments:
Post a Comment