Magufuli asikitishwa kifo mwanafunzi NIT, aagiza hatua za kisheria zichukuliwe....soma habari kamili na matukio360....#share
Na mwandishi wetu, Dar es salaam
RAIS John Magufuli ametoa pole kufuatia kifo cha mwanafunzi
Akwilina Akwilini na ameagiza vyombo vya dola kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika.
Mwanafunzi huyo wa chuo cha usafirishaji Tanzania (NIT) alipigwa risasi akiwa ndani ya daladala jijini Dar es salaam siku ya Ijumaa majira ya jioni, ikiwa siku moja kabla ya uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la kinondoni kufanyika.
Ametoa pole hizo kupitia ukarasa wa twita:
RAIS John Magufuli ametoa pole kufuatia kifo cha mwanafunzi
Akwilina Akwilini na ameagiza vyombo vya dola kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika.
Mwanafunzi huyo wa chuo cha usafirishaji Tanzania (NIT) alipigwa risasi akiwa ndani ya daladala jijini Dar es salaam siku ya Ijumaa majira ya jioni, ikiwa siku moja kabla ya uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la kinondoni kufanyika.
Ametoa pole hizo kupitia ukarasa wa twita:
Kifo hicho kilifuatia baada ya kuibuka makabiliano kati ya jeshi la polisi na wafuasi wa chama cha Chadema
Walioshuhudia wanasema kuwa maafisa wa polisi walitumia vitoa machozi na risasi katika harakati za kuwatawanya mamia ya wafuasi wa chama cha Chadema waliokuwa wakiandamana hadi afisi za tume ya uchaguzi.
Baadhi ya wanachama wa chama hicho walikamatwa.Mwili wa msichana huyo ulikuwa na jeraha la risasi kichwani
No comments:
Post a Comment