Magufuli: Ninawafuatilia majaji wanaokula raha nje ya nchi.....soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu, Dar es
salaam
RAIS John Magufuli ametoa ya
moyoni kuwa anafuatilia mienendo ya baadhi majaji na ameitaka Takukuru, jeshi
la Polisi na Magereza kuhakikisha wanawafukuza watendaji wasio waadilifu kwa
maslahi ya umma
Pia amesema atahakikisha anakomesha uzembe wa makusudi unaofanywa na wanasheria wa serikali katika kesi mbalimbali inayokabilina nazo na kushindwa na kwamba Februari hii majibu ya suala hilo yatapatikana.
Rais John Magufuli
Amesema hayo leo jijini Dar
es salaam kwenye maadhimisho ya wiki ya sheria nchini na kwamba usheleweshwaji
wa kesi bado ni tatizo.
"Wengi wa majaji wanaomba
vibali kwa ajili ya likizo kwenda nje ya
nchi ikiwamo Afrika Kusini na Ulaya na wanakaa kwa siku 28 hadi 30. Ninafuatilia
kwa makini ili nijue wanatoa wapi fedha za kugharamia safari hizo kwa kuwa
mishahara yao ninaifahamu,’’ amesema na kuongeza ‘’Polisi na Mahakama zijiulize
kwa nini zinaongoza kwa vitendo vya rushwa kulingana na utafiti wa Twaweza.’’
Amesema suala la majaji hao ameshamuuliza jaji mkuu, Profesa
Ibrahim Juma lakini hata yeye alikosa
majibu sahihi ya kumjibu.
Rais amesema pamoja na
mafanikio yaliyopatikana katika sekta ya
sheria lakini uadilifu umepungua kwa
watumishi wachache wa mahakama, Polisi, Takukuru na kuwa hawapaswi kuwachwa kwa kuwa ndio wanaodai
rushwa wanabambikiza kesi wananchi, na kutoa hukumu kwa upendeleo.
Amesema kupitia tume ya
utumishi wa mahakama, mahakimu 27 wamestaafishwa
kwa manufaa ya umma kutokana na kufikishwa mahakamani kwa tuhuma mbalimbali japo
walishinda kesi zao na mahakimu wengine
14 na watumishi 67 wa mahakama
wamefukuzwa kazi.
"Polisi, Takukuru, Magereza
igeni mfano wa jaji mkuu kwa kustaafisha watendaji wasiokuwa na uadilifu,
nilitarajia nanyi mngekuja na majina ya mliowafukuza kazi kutokana na kukosa
uadilifu,’’ amesema
Kuhusu
serikali kushindwa kesi mbalimbali rais amesema serikali inashindwa mashauri yake
kutokana na ‘weekness’ kutoka ofisi ya mwendesha mashtaka wa serikali (DPP) na
kwamba watendaji wazuri wanapelekwa katika ofisi yake (Ikulu) na kwamba kabla
ya mwezi Februari kumalizika atatatua changamoto hiyo.
Akitolea mfano rais Magufuli
amesema jumla ya kesi 139 zinazohusiana kodi za kuanzia mwaka 2009 hadi 2015 zenye thamani bilioni 169.1
hadia sasa hazijapatiwa ufumbuzi.
"Lakini zingepatiwa ufumbuzi uenda serikali
ingeshinda baadhi ya kesi na ingepata
fedha,’’ amesema
Pamoja na mambo mengine ameagiza
mapungufu yaliyojitokeza katika sekta ya sheria yaweze kutafutiwa ufumbuzi na ndio lengo lake la
kukubali mfumo wa kisasa wa uendeshaji kesi kwa njia ya Tehama kwa kuwa itaongeza kasi ya utoaji haki,
kudhibiti uzembe na kupunguza gharama za uendeshaji katika mahakama.
Kuhusu
jeshi la Magereza amelitaka
kujitegemea kwa kubuni mbinu
mbadala ikiwamo kuwatumia wafungwa
kuzalisha na kuwabadilisha tabia.
"Jeshi la Magereza lianze
kujitegemea sasa kwa kuwatumia wafungwa kwa kuwafanyisha kazi zenye tija na
kwamba wafungwa wajifunze vizuri ili wabadilike wanapotoka,’’ amesema
Katika
hatua nyingine rais Magufuli amesema anajitathmini kuhusu utendaji wa watendaji anaowateua.
Amesema hatua hiyo ni
kutokana na baadhi ya watendaji serikalini wanakwamisha baadhi ya mambo ikiwamo
kuchelewesha kanuni za sheria kwa takribani miezi tisa tangu asaini sheria.
"Nitajitathimini kuhusu
watendaji ninaowateua na kwamba kanuni za sheria zimekaa kwa takribani miezi
tisa hivyo ninakuagiza waziri wa katiba na
sheria, Profesa Kabudi katika
mwezi huu wa Februari ziwe zimekamilika.’’
No comments:
Post a Comment