Morgan Tsvangirai wa Zimbabwe yupo 'mahututi'......soma habari kamili na matukio360...#share

Na mashirika ya kimataifa
Kiongozi wa upinzani nchini Zimbabwe Morgan Tsvangirai yuko hali mahututi katika hospitali moja nchini Afrika Kusini.
Morgan Tsvangirai 
Vyombo vya habari vimenukuu vyanzo katika familia yake vilivyosema kuwa kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 65 ambaye anatibiwa saratani ya tumbo anakabiliwa na upungufu wa uzani , kuchoka na mishipa yake ya damu kuwa membamba.
Wakati wa harakati zake dhidi ya aliyekuwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe , amepigwa na kufungwa jela mara kadhaa.
Tsvangirai ndiye kiongozi wa chama cha upinzani cha MDC nchini Zimbabwe.
Amekuwa akipelekwa hospitali mara kwa mara tangu mwezi Juni, akipokea tiba katika hospitali moja ya saratani mjini Johannesburg.
Alirejea hospitalini humo mwezi uliopita.
Afya ya  Tsvangirai ilidhoofika kwa haraka siku ya Jumatatu , kulingana na duru za familia zilizozungumza na mtandao wa Bulawayo24 siku ya Jumanne.
Alipoteza hamu ya kula na akawa na tatizo kubwa la kula ama hata kumeza maji, duru zilisema.
 Tsvangirai pia ameripotiwa kuwa na tatizo la kupumua.
Wakati huohuo Duru za MDC zimesema kuwa Tsvangirai yuko hali mahututi na kwamba watu wanafaa kutarajia lolote lile.
Hata hivyo msemaji wa Tsvangirai, Luke Tamborinyoka alisema kuwa kiongozi huyo wa MDC yuko hali nzuri lakini taifa linafaa kumuombea.
Hospitali ambayo  Tsvangirai anatibiwa haijatoa tamko lolote kuhusu swala hilo.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search