Serikali kuanza kuweka alama za mipaka ya kimataifa...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Mara

NAIBU Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya makazi Angelina Mabula amesema Serikali itaanza kuweka alama za mipaka ya kimataifa katika mipaka yake na nchi jirani ya Kenya na Uganda kuanzia machi mwaka huu.
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula na Mkuu wa Wilaya ya Tarime Glorious Luoga wakiwa katika picha ya pamoja na Askari  wa Kenya  wa hifadhi ya Masai Mara ambayo inapakana na hifadhi ya Serengeti wakati  alipokagua mpaka baina ya Tanzania na Kenya  eneo la Serengeti Wilaya ya Tarime mkoa wa mara.

Hatua hiyo inafuatia baadhi ya alama za mipaka yake na nchi jirani katika maeneo mbalimbali  kuharibika ama kuchezewa na hivyo kuleta mkanganyiko baina ya Tanzania  na nchi hizo  ni wapi mwisho wa mipaka.

Akizungumza katika ziara yake mkoani Mara, Mabula amesema kwa sasa fedha kwa ajili ya kazi hiyo imeshatengwa na kinachosubiriwa ni kuanza rasmi kwa kazi hiyo hapo machi mwaka 2018.

‘’katika zoezi la kuweka alama za mipaka vitawekwa vigingi kila baada ya umbali wa mita mia moja sambamba na kubainishwa eneo la ardhi huru’’ alisema Mabula.

Kwa mujibu wa naibu waziri huyo, tayari timu ya wataalamu kutoka nchi za Kenya Uganda na Tanzania zimeshakutana na kukubaliana kuhusiana zoezi la uainishaji mipaka ya  nchi hizo.

Amesema kwa sasa alama zitawekwa katika mipaka iliyopo mikoa ya Mara, Arusha, Kilimanjaro na Tanga na baadaye zoezi litaendelea katika maeneo mengine ya mipaka.

Amesema, ni imani yake baada ya kukamilika kwa zoezi la kuweka alama za kimataifa za mipaka suala la migogoro kuhusiana na mipaka litakwisha.

Kwa mara ya mwisho zoezi la kuweka alama za mipaka ya kimataifa baina ya Tanzania na nchi jirani lilifanyika mwaka 1975 baada ya lile la awali la Tangazo la Serikali (GN) mwaka 1965 kuhusiana na mipaka.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Tarime Grorious Luoga alimueleza naibu waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuwa, mbali na suala la mipaka ya kimataifa wilaya yake inakabiliwa na changamoto ya mipaka baina ya hifadhi ya Serengeti na wananchi wanaozunguka hifadhi hiyo kwani wamekuwa wakivamia na kujenga ndani ya hifadhi na wakati mwingine kuingiza mifugo.

Katika ziara yake ya kukagua mpaka wa Tanzania na Kenya katika eneo la Serengeti, Naibu Waziri wa Ardhi, nyumba na Maendeleo ya Makazi Mabula alifuatana na Mkuu wa Wikaya ya Tarime Glorious Luoga pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Upimaji Vijijini kutoka Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Huruma Lugalla ambapo kwa pamoja walijionea hali halisi ya mpaka wa Tanzania na Kenya na baadhi ya alama za mipaka zilizoharibika




About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search