Wadaiwa SIDO wapewa siku 14....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

KAMPUNI ya udalali ya Yono Auction Mart imetoa siku 14 kwa wadaiwa sugu wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO),  kulipa madeni yao kabla ya chukuliwa hatua za kisheria ikiwamo mali zao kupigwa mnada kufidia deni.
Meneja wa SIDO mkoa wa Dar es Salaam Macdonald Maganga akizungumza na waandishi wa habari.

Hatua hiyo imetangazwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo, Scholastica Kevela akizungumza na waandishi wa habari wakati SIDO ilipokuwa ikizindua kampeni ya kukusanya madeni kwa wateja wao.

“Kwa wadaiwa wote wa SIDO, wanaoishi kwenye viwanda na nyumba za SIDO bila kulipa pango, waliochukua mikopo na hawataki kurejesha kwa sababu wanazozijua wao, mkono wa Yono uko kazini ni vyema wakachukua hatua wakalipa ili kuondosha usumbufu,” amesema Kevela.

Meneja wa SIDO mkoani Dar es salaam, Macdonald Maganga amesema wadaiwa  ni wale waliopewa maeneo maalumu ya viwanda kwa ajili ya kufanyia kazi zao na waliopatiwa huduma ya fedha kwa mkopo na kushindwa kurejesha kwa wakati.

“Kuna ambao wamekaa miaka mingi au miezi mingi bila kurejesha fedha kwetu kama shirika inatuathiri kwa sababu hatuwezi kuwahudumia wengine,” amesema Maganga.

Maganga amesema wanadai jumla ya sh.milioni 350 kutoka kwa wadaiwa  zaidi ya 77.

Mdaiwa Masoud amedai hawafanyi makusudi kutolipa madeni  ni kutokana na kodi kupanda kila mwaka huku hali ya biashara ikiwa mbaya.

“Ukizingitia soko la ushidani na hali ya bidhaa unashindwa kuuza kwa wakati kwa hiyo tunalipa lakini hatulipi kwa wakati,” amesema.


Amedai wamepangishwa kwa zaidi ya miaka 40 wakifanya shughuli zao na kama wangekuwa hawalipi kwa kipindi chote  wangefukuzwa hivyo ameiomba serikali kutodhani kuwa wanapuuza kulipa madeni.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search