Nondo apandishwa kortini, arudishwa mahabusu...soma habari kamili na matukio360...#share



Na mwandishi wetu, Iringa

Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Iringa imezuia dhamana ya Mwenyekiti wa Mtandao wanafunzi vyuo vikuu, Abdul Nondo kwa sababu za usalama wake kwa madai kuwa bado maisha yake yapo hatarini na amerudishwa mahabusu.


Abdul Nondo akiwa chini ya ulinzi wa polisi

Akizuia dhamana hiyo hakimu mkazi wa mahakama ya Iringa John Mpitanjia amesema anaomba muda wa kupitia vifungu vya sheria hadi Machi 26,mwaka huu ili kujiridhisha maisha yake hayatakuwa hatarini kama mtuhumiwa akipatiwa dhamana.

Abdul Nondo anatuhumiwa kwa makosa mawili ambapo kosa la kwanza ni kuchapisha taarifa za uongo mtandaoni ambapo inaelezwa kuwa Machi 7 mwaka huu akiwa Ubungo alichapisha na kusambaza taarifa kwa kutumia mtandao WhatsApp kuwa yupo hatarini.

Shtaka la pili ni kutoa taarifa za uongo kwa mtumishi wa umma Mafinga alipokuwa anatoa taarifa kwa askali katika kituo cha polisi Mafinga na kusema kuwa alikuwa ametekwa na watu wasiojulikana Dar es salaam na kupelekwa kiwanda cha pareto Mafinga.

Mshtakiwa amekana mashtaka yote na amerudishwa mahabusu hadi Machi 26 atakapofikishwa tena mahakamani kwa ajili ya kusilikiliza maamuzi ya mahakama juu dhamana.


About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search