Serikali: Wanafunzi wapime TB kabla kuingia shule...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, amepiga marufuku wanafunzi kujiunga na shule za bweni bila kupima ugonjwa wa kifua kikuu (TB).
Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiwa amemgeukia mmoja wa watoto mwenye tatizo la ugonjwa wa kifua kikuu akiwa anakunya dawa iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam.

Amepiga marufuku hiyo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa  akizungumza na wadau wa afya katika uzinduzi wa dawa ya watoto ya ugonjwa huo (New TB Paediatric Formulation) pamoja na kukabidhi mashine tano (Genexpert Machines) kwa hspitali binafsi kwa ajili ya kusaidia kutoa hudua ya vipimo vya ugonjwa huo.

“Hakuna mwanafunzi ataingia katika shule ya bweni bila kupimwa ugonjwa wa kifua kikuu, narudia kutoa maelekezo kwa waganga wafawidhi zile fomu za afya wanatakiwa wafanye uchunguzi na siyo kutia saini tu, nakusema tumemuangalia yuko sawa, tutawaua watoto wetu kama hatutachukua hatua ya kupambana na ugonjwa wa kifua kikuu,” amesema Ummy.

Waziri Ummy amesema kwa mujibu wa makadirio ya mwaka 2016 watu takribani laki 160,000 huwa na matatizo ya ugonjwa wa kifua kikuu nchini kila mwaka ambapo kati ya hao watoto ni 6457.

Amefafanua kuwa katia ya wagonjwa hao laki 160,000 ni watu takribani 65900 tu ambao waliweza kufikiwa na kuwekwa kwenye mpango wa matibabu.

Amesema TB ni miongoni mwa magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha vifo vingi, kwa mujibu wa shirika la afya duniani (WHO) mwaka 2016 takribani watu milioni 1.3 walifariki dunia kutokana na ugonjwa huo.

“Na hapa nchini kwetu kwa takwimu ambazo tunazo zinaonesha kwamba jumla ya vifo vinavyotokea miongoni mwa hao ambao wanamatatizo ya kifua kikuu kwa mwaka ni vifo 28000 sawa na vifo 77 kila siku,” amesema.

Amiongeza kwamba kwa mujibu wa takwimu pia za WHO inakadiriwa kuwa zaidi ya watu milioni 10.4 huugua ugonjwa huo kila mwaka ambapo milioni 1 kati ya hao ni wa toto wa chini ya umri wa miaka 14.

Amesema asilimia 90 ya watu 100 wanaokwenda hospitali na kupata matibabu , watu 90 wanapona kabisa hivyo changamoto ni jinsi ya kuwapata wagonjwa ncnini na kuweza kuwaingiza kwenye mfumo wa matibabu.

Akitaja hospitali zilizokabidhiwa mashine hizo kwa ajili ya kufanya vipimo na kuibua wagonjwa wapya ni Aga Khan, Kairuki, Regency, TMJ na Shree Hindu Mandal.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search