Utelezi, kona kali chanzo ajali ya treni....soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu, Kigoma

TAARIFA za awali zimeeleza utelezi na kona kali ndio chanzo cha ajali ya treni ya abiria iliyokuwa safarini kutoka Dodoma kwenda Kigoma kupitia Tabora.

Takriban watu 29 wamejeruhiwa katika  ajali hiyo iliyotokea jana  mchana eneo la kijiji cha Mpeta, wilayani Uvinza mkoani Kigoma.

Ajali hiyo imesababishwa na kichwa cha treni kuacha njia na mabehewa mawili kuanguka.
Kaimu meneja wa wamawasiliano wa Shirika la Reli la Tanzania (TRL) Mohamed Mapondela ameambia matukio360 kuwa; "Sababu za awali za ajali hiyo kupitia timu yetu ya kutathmini ajali ni utelezi na kona kali," amesema.
Ajali ilitokea majira ya saa saba na dakika hamsini mchana eneo la katikati ya stesheni ya Malagarasi na Uvinza.
"Tathmini kamili ya ajali itatolewa pale ambapo mabehewa yatakuwa yameinuliwa."
Mapondela amesema eneo hilo si kwamba ni baya na halina historia ya kupata ajali yoyote ile.
Mbunge wa Kigoma mjini, Zitto Kabwe ameandika kwenye Facebook kwamba amezungumza na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma na kufahamishwa kwamba chanzo cha ajali ni injini kupoteza njia kufuatia mchanga uliokuwa kwenye njia ya reli. "Naomba uchunguzi ufanyike ili kuona kama mchanga ule ni sababu ya mvua kubwa zinazonyesha ama la. Treni ndio usafiri wa wanyonge wengi mkoani kwetu hivyo ajali za namna hii zinastusha na kuogopesha. Natoa pole sana kwa wana Kigoma na Watanzania wengine," amesema.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search