BENKI YA TPB Pls YAWEKA REKODI KIUTENDAJI, SASA MTAJI WAKE WAFIKIA SHILINGI BILIONI 60...SOMA HABARI KAMILI NA MATUKIO360...#SHARE
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
OFISA Mtendaji Moshingi aipongeza Serikali
kwa uamuzi wa benki hiyo kuunganishwa na Twiga Bancorp.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya TPB Pls Sabasaba Moshingi
(kushoto) akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani Dar es Salaam
jana,wakati akitoa shukrani kwa Serikali kutokana na uamuzi wa
kuinganisha benki hiyo na Benki ya Twiga Bancorp.Kulia ni Mkurugenzi wa
Teknohama na Uendeshaji wa Benki ya TPB Jema Msuya.
BENKI ya TPB Pls imesema
imeweka rekodi nzuri ya utendaji katika kipindi cha miaka 6 iliyopita ambapo
hadi sasa mtaji wake umeongezeka kutoka Sh. bilioni 8 mwaka 2010 hadi kufikia
zaidi ya Sh.bilioni 60.
Imefafanua aidha kwa mwaka
2017, benki ya TPB ilitoa gawio la zaidi ya Sh. bilioni moja kwa Serikali
ambaye ndiye mwenye hisa nyingi.
Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na
Ofisa Mtendaji Mkuu wa benki hiyo Sabasaba Moshingi wakati anatoa shukrani zake
kwa Serikali kutokana na uamuzi wake wa kuamua kuiunganisha benki hiyo na
pamoja na Benki ya Twiga Bancorp.
Akifafanua kuhusu benki hiyo amesema
katika kuendelea kutekeleza majukumu yao benki ya TPB kwa mwaka 2017 ilipata
faida kabla ya kodi ya Sh.bilioni 18.4 ikilinganishwa na faida ya Sh.bilioni 15.7
iliyopatikana mwaka 2016.
Amesema matokeo hayo ya awali kwa robo ya
kwanza ya mwaka 2018 inaonyesha mwaka huu faida inaweza kuongezeka zaidi ya
kiwango cha mwaka jana.
"Tunatoa shukrani kwa Serikali ya
awamu ya tano kwa kutuamini benki ya TPB kwa kazi tunayofanya kwa raia wa
Tanzania, na tunahaidi tunaongea ufanisi zaidi, na kuwafikia walengwa wote
katika jamii yetu,"amesema.
Kuhusu benki hiyo kuunganishwa
na benki ya Twiga Moshingi amesema Mei 17 mwaka huu Benki Kuu ya Tanzania(BoT)
kwa niaba ya Serikali, imeamua kuziunganisha benki hizo na kuunda benki
madhubuti itakayojulikana kama benki ya TPB na kusisitiza kuunganishwa kwa
benki hizi mbili kunatokana na kutetereka kwa mtaji wa benki ya Twiga.
Moshingi amesema anaishukuru
Serikali kwa kuiamini benki ya TPB pamoja na menejimenti yake, na kuamua
kuziunganisha benki hizo ili kupata benki moja yenye nguvu na kuongeza ufanisi.
Amesema kuunganishwa kwa benki
hizo kunazaa benki moja imara ya TPB Bank Plc, ambapo wafanyakazi, wateja,
amana pamoja na rasilimali zote zilizokuwa za Twiga Bancorp zitahamishwa kwenda
TPB Bank Pc.
"Nachukua fursa hii kuwatoa hofu
wateja wote waliokuwa na amana zao kwenye benki ya Twiga kuwa wasiwe na hofu
kwani amana zao ziko salama kabisa, na wataendelea kupata huduma zote za
kifedha kupitia kwenye matawi yao ya Twiga kwa muda, wakati taratibu
zinafanyika ili kupata huduma hizo kwenye matawi yetu benki ya TPB mara baada
ya taratibu ya kuunganishwa kwa mifumo ya benki hizi mbili utakapo
kamilika,"amefafanua.
Moshingi ameongeza kuwa hata hivyo mashine
za kutolea fedha za benki hizo mbili ziko kwenye mtandao mmoja na hivyo wateja
wake wote wataendelea kupata huduma kama kawaida.
Mkurugenzi wa Teknohama na Uendeshaji wa Benki ya TPB Pls
Jema Msuya(kushoto) akibadilisha mawazo na baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo
leo jijini Dar es Salaam baada ya Ofisa Mtendaji Mkuu wao Sabasaba Moshingi
kumaliza kikao kati yake na waandishi wa habari ambacho kilikuwa na lengo la
kutoa shukrani zao kwa Serikali kwa uamuzi wa kuiunganisha benki hiyo na Twiga
Bancorp.
No comments:
Post a Comment