Mbowe atoa kauli madiwani 46 chadema kuhamia CCM...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Taifa (Chadema) Freeman
Mbowe amefunguka na kutoa neno kuhusu madiwani 46 ambao wamejiuzulu nafasi zao
na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kusema kuwa jambo hilo linafanywa
na CCM kwa lengo la kuwakatisha tamaa wana Chadema
Mbowe amesema kuwa wapo watu wanadhani kitendo cha baadhi ya
madiwani kuhama chama hicho na kwenda CCM ni kukiuwa chama hicho na kusema
suala hilo haliwezi kutokea kwani madiwani wa Chadema nchi nzima wapo zaidi ya
1130 huku madiwani 46 ndiyo waliohama na kwenda CCM na kusema kitendo hicho
kinawapa funzo katika maandalizi ya kutafuta viongozi ambao kweli wanaweza
kukisimamia chama na si wale wanaotafuta fursa za kutoka kupitia uongozi.
"Kazi kubwa inayofanywa na CCM ni kuwakatisha tamaa na
jambo ambalo limefanyika karibuni ambalo linaonekana wana CHADEMA wengi
wamerudishwa nyuma basi ni suala la madiwani.
"Madiwani wamenunuliwa jamanii wanaunga mkono juhudi, kuna
watu wengine ni mizigo lakini sasa tunafanyaje lakini watu wa CHADEMA wanakata
tamaa eti madiwani wanaisha chama kinakufa
"Hiki chama hakifi mzee CHADEMA nchi nzima ina madiwani
1184 madiwani mpaka dakika hii wameondoka ni madiwani 46 kwa hiyo tuna madiwani
zaidi ya 1130 wamebaki CHADEMA halafu mtu anasema CHADEMA inakufa una akili
wewe?"
Aidha Mbowe amesema kuwa hao viongozi ambao wanahama kutoka
CHADEMA na kwenda CCM kwao ni kama funzo kwamba wapo viongozi na watu
mbalimbali ambao wapo ndani ya CHADEMA kwa lengo la kutafuta fursa tu na
wanapoikosa hiyo fursa na ulaji wanaamua kuondoka.
"Kwetu ni funzo tunapojiandaa kwenda kwenye uchaguzi wa
Wenyeviti wa Mtaa, Vijiji, madiwani, wabunge hata nafasi ya Urais tukajiandaa
na kina nani wanaoishi ndoto ya CHADEMA lazima safari hii tujiridhishe mapema
huyu tukimpa nafasi basi historia yake tunaijua vyema" alisema Mbowe
No comments:
Post a Comment