Tanzania yashika nafasi ya 7 kuvutia wawekezaji Afrika...soma habari kamili na matukio360...#share


Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

KITUO cha Uwekezaji nchini (TIC) kimesema Tanzania imeendelea kushika nafasi nzuri ya kuvutia uwekezaji katika nchi za Afrika ambapo kwa mwaka jana 2017 imeshika nafasi ya saba kati ya nchi 10 za Afrika zenye ushawishi wa kuwavutia wawekezaji.
Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Geoffrey Mwambe akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari  leo jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa TIC Geoffrey Mwambe, amesema hatua hiyo ni kubwa kutokana na akuendelea kupanda kutoka nafasi ya 11 mwaka 2014 hadi nafasi ya 9 mwaka 2016.

“Na hii naomba sana kusisitiza mwekezaji asiende kutafuta huduma kwenye taasisi zingine za serikali aje TIC atapata huduma zote ambazo anazihitaji kutoka TIC, kwa sababu tunao maafisa wa hizo taasisi zingine ndani ya TIC,” amesema Mwambe.

“Sasa kuonesha kwamba tumedhamilia kuwafikia wananchi lakini pia na wawekezaji wakiwemo watanzania mpaka kukamilika kwa utekelezaji wake ambao unakuwa ni miaka kuanzia sasa huwa tunatoa miaka mitatu,” ameongeza.

Aidha amesema kuwa katika kipindi cha miezi minne kituo kimefanikisha kuandikisha miradi mipya 109 inayotarajia kutengeneza fursa za ajira kwa vijana 18,172.

Mwambe ameongeza kwamba thamani ya miradi hiyo iliyosajiliwa kama itatekelezwa kama ilivyokusudiwa itagharimu Dolla za Kimarekani milioni 13, 342.21.

“Kama mnavyofahamu ni kwamba mwitikio mkubwa ni waviwanda kwa hiyo bado eneo la viwanda limeweza kutoa uwekezaji mwingi zaidi,” amesema .

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uhamasishaji Uwekezaji wa kituo hicho John Mnali amesema miundombinu kama umeme na barabara ni changamoto kwa wawekezaji hivyo serikali inaendelea kulishughulikia na kuboresha mazingira ya uwekezaji ili uendelee kuongezeka siku hadi siku.

“Kuna miradi kadhaa ya serikali ambayo inaendelea kwa upende wa Tanesco ya kuweza kuzalisha umeme na kuhakikisha kwamba umeme unaozalishwa unakidhi mahitaji ya wawekezaji,” amesema Mnali.

“Na kama mnavyoona ongezeko la miradi inayoingia imekuwa mingi zaidi ukilinganisha na mahitaji ya umeme, yaani ukilinganisha na umeme uliopo, kwa hiyo kunakuwa na umuhimu wakuwa na miradi mikubwa ya umeme ili uzalishaji huo wa umeme uweze kukidhi mahitaji yote ya wawekezaji wa sasa na wale wanaotarajia kuja,” ameongeza.

Amewataka wawekezaji wandani na nje wanaokusudia kuwekeza miradi yao nchini wawekeze kwani changamoto hizo zinaendelea kupatiwa ufumbuzi.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search