"Watu wasiojulikana" wawa gumzo bungeni...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MATUKIO ya utekaji  na kupotea kwa watu yameibua mvutano baina ya wabunge, bungeni leo.

 Mvutano huo ulianza wakati mbunge wa Tabora Kaskazini (CCM), Almas Maige akichangia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya mwaka 2018/19 ya Sh945.5 bilioni.

Katika mchango wake, Maige amegusia suala la matukio ya watu wasiojulikana akisema;

 “Watu wasiojulikana hawa wanaosemwa na wenzetu wa upinzani na huenda watu wasiojulikana wanasema wanafanya kazi upande wa upinzani tu hapana. Mimi nina orodha ya wana CCM waliofanyiwa na watu wasiojulikana.”

Kauli hiyo haikupita hivi hivi, kwani mbunge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara alisimama kumpa taarifa Maige akisema idadi ya watu waliotendewa uhalifu na watu wasiojulikana ni wengi, “Kuna utekaji, uonevu katika nchi hii.”

Mwenyekiti wa Bunge, Najma Giga akamuuliza Maige, “Unapokea taarifa hiyo ya mheshimiwa Waitara.”

Kabla hajajibu, Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Mwigulu Nchemba akasimama na kusema jeshi la polisi halijateka watu; “Mheshimiwa Maige anaongelea watu wasiojulikana.”

Hoja haikuishia hapo, Mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia naye akasimama na kusema, “Suala la uhalifu, halilinganishwi kwa vyama vya siasa, sisi sote ni Watanzania na jeshi la polisi linalinda usalama wa raia wote.”

Hapo ndipo Maige akapewa fursa na Mwenyekiti Giga kuendelea kuchangia akisema;

 “Mimi siongelei uhalifu, naongelea watu kufanya matukio na hawakamatwi. Mimi nasema watu wanaofanya matukio wakamatwe.”

Bado mvutano uliendelea kwani, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Kunti Yusuph akasimama kumpa taarifa Maige kwa kusema;

 “Suala la kusema matukio yaliyofanyika upande wa upinzani na CCM hayafanani, inadhihirisha kwamba Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake imebariki mfumo na matukio haya ili waje waseme Chadema ni wachache na CCM ni wengi. Asante amedhihirisha.”

Akihitimisha mchango wake kwa eneo hilo, Maige amesema, “Mimi nashangaa upande ule (wa upinzani) wanakurupuka, mimi naongelea ombi langu kwa Serikali ili kuweza kuwakamata watu wasojulikana.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search