DUA YA SHEIKH #ALHADI #MUSA KWA ALIEKUA ‘BOSS WA FREEMASON’ SIR #ANDY #CHANDE IMEENDELEA KUZUA HISIA TOFAUTI MIONGONI MWA WAUMINI WA DINI YA KIISLAMU NCHINI.














Kufuatia Sheikh Mkuu wa Dar es salaam, kusoma dua maalum ya kumwombea marehemu Andy Chande (pichani) ambaye ni mwenyekiti wa freemason Afrika Mashariki.  aliyeaminika kuwa na imani kinzani wiki iliyopita imezua maswali miongoni mwa waumini wa dini ya kiislamu.
Sheikh mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam alisoma dua hiyo maalum ya kuwakumbuka waasisi wa shule hiyo na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali akimbo Rais Msaatafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin William Mkapa sanjari na wanafunzi wengine waliowahi kusoma katika shule hiyo.
Sir Andy Chande alifariki dunia, Aprili 7, mwaka huu nchini Kenyaalikokuwa akipatiwa matibabu na kuzikwa katika Makaburi ya Baniani, Makumbusho jijini hapa kwa kuchomwa moto.
Katika enzi za uhai wake, Sir Andy Chande aliwahi kuweka wazi kuwa yeye ni mfuasi na kuhani mkuu wa Jumuiya ya Freemason, jumuiya ambayo inaaminika na baadhi ya watu kwamba iko kinyume na mafundisho ya dini za Kiislamu na Kikristo. Katika tukio hilo la kuwakumbuka waasisi wa shule hiyo, Shehe Alhadi aliongoza dua maalumu kwa upande wa dini ya Kiislamu kwa ajili ya kumwombea marehemu Chande jambo lililoibua mjadala mkubwa.
Baadhi ya watu walihoji kuwepo kwa shehe mkuu wa Dar kwenye dua hiyo wakati marehemu alijulikana kuwa ni Freemason ambayo wengi hawaiamini kama ina sera za Mungu. Msikie huyu:
“Mimi binafsi sidhani kama ni sahihi kumfanyia dua mtu ambaye aliwahi kuweka wazi kwamba yeye yupo upande wa kushoto, tena akiwa mwenyekiti na kuhani mkuu wa jumuiya ambayo inaaminika inakwenda kinyume na maadili ya Kimungu,” alisema Kimashi John kupitia ukurasa wake Facebook.
Mbali na Kimashi mijadala mingi iliyotawala mitandaoni siku ya tukio hilo ilikuwa ni uwepo na uwakilishi upande wa dini ya kiislamu wa sheikh Alhadi katika hafla hiyo
Gazeti moja maarufu kwa maswala ya udaku (Uwazi) baada ya kuyasikia hayo, liliamua kumtafuta Shehe Alhadi mwenyewe ili kutoa ufafanuzi juu ya suala hilo.
Akizungumza na mwandishi wetu kwa njia ya simu, Shehe Alhadi alikuwa na haya ya kusema:
“Katika dua niliyoiomba siku ile hakuna neno nililosema kwamba Mungu aiweke roho ya marehemu Chande mahali pema peponi. Unaweza kusikiliza tena rekodi za ile dua, nilichokifanya ni kumwombea kwa Mwenyezi Mungu amlipe kwa mambo yote aliyoyafanya duniani maana yeye ndiye hakimu wa mwisho.”

Aidha, katika hatua nyingine Uwazi lilipotaka kujua kama alishawahi kumpa elimu ya dini ya Kiislamu, marehemu Sir Chande ikiwa ni pamoja na kumtaka asilimu, Shehe Alhadi hakuwa tayari kulizungumzia hilo zaidi ya kukiri kwamba amekuwa akifahamiana na marehemu kwa muda mrefu.

credit:blessnewstz

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search