#Emmanuel Macron aibuka kidedea Uchaguzi Mkuu Ufaransa ! amuacha mbali mpinzani wake

MGOMBEA huru wa Urais nchini Ufaransa, Emmanuel Macron, (39), anakuwa rais wa kwanza kijana katika historia ya nchi hiyo, kufuatia ushindi wake baada ya kujipatia asilimia 66.06 ya kura zote zilizopigwa dhidi ya asilimia 33.94 alizopata mgombea wa chama cha National Front, Bi Marine Le Pen (48).




Bw. Macron ambaye miaka mitatu iliyopita hakuwa akijulikana miongoni mwa Wafaransa wengi ameshinda katika uchaguzi huo wa awamu ya pili uliofanyika Jumapili Mei 7, 2017.
Shamra shamra, kelele na vifijo vililipuka miongoni mwa wafuasi wake ambapo katika hotuba yake, Rais huyo kijana alisema jukumu lake kubwa ni kuliunganisha taifa la Ufaransa ambalo liligawanyika, na kwamba dunia nzima ilikuwa ikifuatilia kwa karinbu uchaguzi huo na wakitusubiri sisi kulinda nuru ya taifa lililokuwa kwenye kitisho kutoka maeneo mengi.
Pamoja na kushindwa kwenye uchaguzi huo, kura alizopata Bi Le Pen zimedhihirisha ushindi wa kihistoria kwa makundi ya kutetea haki nchini Ufaransa.
Katika hotuba yake ya kukubali matokeo, Bi. Le Pen alisema yeye alikuwa kiongozi wa “jeshi” kubwa la upinzani na kuapa kukifanyia mabadiliko makubwa chama chake.
Hata hivyo idadi ya wapiga kura ilikuwa ndogo kupindukia katika historia ya chaguzi nchini humo kwa miaka 40 iliyopita.
Habari ya awali


Mgombea Urais kijana nchini Ufaransa, Emmanuel Macron,(39) ameshinda kwenye uchaguzi wa urais wa nchi hiyo wa mkondo wa pili uliofanyika  Jumapili Mei 7, 2017. Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya kimataifa,  Macron amembwaga mwanamama Marine Le Pen baada ya kujipatia asilimia 66.06% ya kura zote zilizopigwa dhidi ya asilimia 33.94, alizopata Bi. Le Pen kutoka chama cha National Front. (AN).

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search