Msimamo wa Ligi Kuu England hadi leo 08/05/2017: Ona Wenger "alivyoishika shati" Man U na kufufua matumaini ya nne bora EPL.

















Washika bunduki wa Jiji la London Timu ya arsenal jana ilichafua record ya Manchester United ya mechi 25 bila kushindwa kwa kuwalaza mashetani wekundu hao wekundu kwa 2-0 mechi ya Ligi Kuu ya England Jumapili.
Ushindi huo uliweka hai matumaini ya Arsenal ya kumaliza katika nafasi nne za kwanza, ingawa bado watatarajia timu nyingine zijikwae.
Mabao ya Arsenal yalifungwa na Granit Xhaka na Danny Welbeck kipindi cha pili.
Licha ya kocha Jose Mourinho kuwaingiza uwanjani Marcus Rashford na Jesse Lingard kujaribu kuokoa timu yake juhudi zake hazikufua dafu..
Matokeo hayo yamewaacha Arsenal wenye mechi moja mkononi wakiwa nafasi ya sita, alama mbili nyuma ya United ambao wanashikilia nafasi ya tano na sita nyuma ya Manchester City ambao wanashikilia nafasi ya nne.


Pamoja na kufufua matumaini ya Arsenal kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, ushindi huo wa Jumapili pia ulisaidia kufifisha rekodi mbaya ya Wenger dhidi ya Mourinho ambapo kati ya mechi 15 Wenger hajawahi kuishinda timu iliyokuwa inanolewa na Mourinho isipokuwa mechi ya Ngao ya Jamii ya mwaka 2015.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search