AFYA YAKO: Unayopaswa kufahamu kuhusu Ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB).. #share
Namna
ya kumtambua mtu anayeugua ugonjwa wa TB
Moja ya chanjo muhimu za mwanzo kabisa
nilizotaja ni chanjo ya kuzuia ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB). Huu ni ugonjwa
hatari ambao unaweza ukamuathiri mtu wa jinsi na rika lolote.
Ugonjwa wa kifua kikuu ni ugonjwa wa kuambukizwa unaosababishwa
na aina mbalimbali za vimelea
vya bakteria ambao hujulikana kama Mycobacterium
tuberculosis. Kifua kikuu ni ugonjwa unaoathiri mapafu, lakini pia ugonjwa huu unaweza kuathiri sehemu nyingine za mwili pia.
Maambukizi
Kifua kikuu husambazwa kutoka kwa mtu mmoja
hadi mwingine kwa njia ya hewa, hasa wakati mtu mwenye maambukizi
anapokohoa au kupiga chafya.
Watu wengi wanaishi na
vimelea vya ugonjwa wa kifua kikuu bila kuwa na dalili zozote kwa miaka mingi,
maambukizi ya aina hii huwa hayana madhara. Lakini baadhi ya watu huweza kupata
dalil za kifua kikuu kama kinga ya mwili itapungua.
Watoto wadogo na wazee ni
makundi ya watu ambayo hupata maambukizi kirahisi zaidi, hii ni kwasababu kinga
ya mwili katika makundi haya ya watu huwa si ya kutosha.
Watu wengine walio katika
hatari ya kuambukizwa ugonjwa wa kifua kikuu ni wale ambao wana magonjwa
yanayosababisha upungufu wa kinga mwilini kama vile Ukimwi na magonjwa ya
saratani.
Ikumbukwe kuwa watoto
hupata maambukizi ya kifua kikuu kwa urahisi sana pale wanapokua karibu na mtu
mzima mwenye maambukizi ya ugonjwa huu.
Dailili zake
Dalili za ugonjwa wa
kifua kikuu ni pamoja na kukohoa kwa muda wa wiki mbili mfululizo au zaidi, homa
za mara kwa mara, kutokwa na jasho jingi hasa nyakati za usiku, kukohoa
makohozi yenye damu na kupungua uzito.
Baadhi ya dalili hizi
zinaweza zisionekane kwa uwazi hasa kwa watoto, hivyo ni muhimu kuhakikisha kama
mtoto anaedhaniwa kuwa na kifua kikuu alishawahi kuishi karibu na mtu mzima
ambaye amegundulika kuugua ugonjwa huo katoka kipindi husika.
Vipimo na Jinsi ya kuutambua
Njia ya kwanza ya kutambua kama mtu ana
maambukizi ya ugonjwa wa kifua kikuu ni kwa dalili alizonazo. Ni muhimu sana
kwa daktari kupata maelezo toka kwa mgonjwa kwa umakini mkubwa ili kuona kama
mgonjwa ana dalili za kifua kikuu.
Njia ya kitaalamu ya utambuzi wa kifua
kikuu ni kwa kutumia X-Ray ya kifua.
Pia wataalamu wa maabara hutumia darubini na kufanya uchunguzi wa vimelea maradhi kutoka katika makohozi na aina
mbalimbali za majimaji ya
mwilini.
Kipimo cha ngozi kijulikanacho kama TST
au Mantoux hutumika zaidi kwa waoto wadogo. Vipo pia vipimo vya damu na vingine
vingi vya kisasa vya kijenetiki. Katika
siku za hivi karibuni, aina fulani ya panya waliofundishwa wamekua wakitumika
kutambua kama makohozi yana vimelea vya kifua kikuu.
Matibabu
na jinsi ya kuzuia
Ugonjwa wa
kifua kikuu unatibika na ni muhimu kama mtu ana dalili tajwa awahi katika kituo
cha afya kwaajili ya matibabu. Baada ya kuhakikisha kwamba mgonjwa ana kifua
kikuu, daktari humuanzishia dawa mgonjwa na kumpa maelezo kuhusu umuhimu wa
kumeza dawa kwa wakati.
Ni muhimu
kuhakikisha kwamba watoto wote waliozaliwa wanaoata chanjo ya kuzuia maambukizi
ya kifua kikuu. Endapo umegundulika kuwa na kifua kikuu, kumbuka kufunika mdomo
na pua unapokohoa na kupiga chafya na kutokutema mate hovyo ili usiwaambukize
watu wengine.
Ni muhimu
uwafahamishe ndugu na marafiki kwamba unaugua kifua kikuu na upo kwenye
matibabu ambayo pia ni lazima yakamilike ili kuzuia hatari ya kupata kifua
kikuu kilicho sugu ambacho matibabu yake ni magumu sana.
Kwa mtu
mwenye kifua kikuu ni muhimu kupata ushauri nasaha kwa ajili ya kupima virusi
vya ukimwi (VVU) kwa sababu magonjwa haya yana uhusiano wa karibu.
Makala hii imeandaliwa na Dk. Pius Muzzazzi
No comments:
Post a Comment