Breaking News: Jamal Malinzi, Rwegamalila na Harbinder Singh.. 'mguu kwa mguu' Mahakamani,.. #share.. warudishwa 'mahabusu'
Mwenyekiti wa TFF Jamal Malinzi na Katibu Mkuu wake Celestine Mwesigwa wamepandishwa kizimbani kwa mara ya pili leo 03/07/2017 kusomewa mashtaka na kisha wamerudishwa mahabusu baada ya kukataliwa dhamana na watafikishwa tena Mahakamani tarehe 17/07/2017.
Wawili hao wanakabiliwa na mashitaka mbalimbali kuanzia 25 hadi 28 likiwemo lile la matumizi mabaya ya ofisi na utakatishaji wa fedha.
Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu, Wilbard Mashauri alisema upande wa utetezi wenyewe wanatambua kuwa mashitaka ya utakatishaji fedha hayana dhamana.
TFF President Jamal Malinzi, Secretary, Celestine Mwesigwa and Cashier, N. Mwanga have been denied bail and remanded until July 17 pic.twitter.com/MiDNugFpLI— The Citizen Tanzania (@TheCitizenTZ) July 3, 2017
Wakati huo huo,.. Mkurugenzi wa kampuni ya VIP Engeneering na mmiliki mwenza wa zamani wa IPTL, James Rugemalira na Habinder Seth Sigh, Mwenyekiti Mtendaji wa PAP wamefikishwa mahakamani leo na kuongezewa mashtaka mengine sita ya kuhujumu uchumi.#HABARI Rais wa TFF Malinzi na Katibu Mkuu Mwesigwa, watapanda kizimbani leo kusomewa mashtaka 28 ikiwa ya utakatishaji wa Fedha na Rushwa. pic.twitter.com/HT3B4LcHGc— East Africa TV (@eastafricatv) July 3, 2017
Awali watuhumiwa hao walipandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kujibu tuhuma ya uhujumu uchumi na kula njama, kughushi, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kuisababisha hasara serikali, lakini watuhumiwa hao leo tena wamepandishwa kizimbani na kuongezewa makosa mengine sita ya ya utakatishaji wa fedha na kufikisha jumla ya mashtaka 12.
Mbali na hilo watuhumiwa hao wamekwama baada ya kukosa dhamana tena na wote wamerudishwa rumande mpaka tarehe 14 Juni mwaka huu ambapo kesi yao itasomwa tena katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam.
Mahakama ya KISUTU yawaongezea Mashtaka mengine 6 Harbender Seth, James Rugemarila na kufikia Mashtaka 12, warudishwa rumande hadi Julai 14 pic.twitter.com/3C3UERjaPL— Radio One Stereo (@RadioOneStereo) July 3, 2017
No comments:
Post a Comment