Abiria watakiwa kuwapeleka Polisi wanaopandisha nauli kiholela...soma habari kamili na matukio

Na Salha Mohamed,Dar es Salaam
BARAZA la Ushauri na Watumiaji wa Huduma za Usafiri wa Nchi Kavu na Majini, limewataka wananchi kutoa taarifa kwa mamlaka husika ikiwamo Polisi endapo watatozwa nauli tofauti na zilizopangwa.

Hatua hiyo inafuatia katika kipindi hiki cha mwezi Desemba nauli hasa kwa wasafiri waendao mikoani wanaotumia usafiri wa mabasi hupanda maradufu.

Katibu Mtendaji ,Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Usafiri wa Nchi kavu na Majini, Dk. Oscar Kikoyo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya usafiri ilivyo katika kipindi hiki cha sikukuu za Krismas na Mwaka Mpya wa 2018.

Wito huo umetolewa  leo jijini Dar es Salaam  na katibu mtendaji wa baraza hilo, Dk Oscar Kikoyo wakati akizungumzia hali ya usafiri katika kipindi cha sikukuu za krismas na mwaka mpya (2018).

"Baadhi ya watoa huduma ambao si waaminifu katika kipindi hiki kama  ni njia ya kuvuna zaidi kutoka kwa watumiaji kinyume na masharti ya leseni zao. Hivyo wasafiri wachukue hatua ya kuwapeleka polisi au katika mamlaka husika za usafirishaji, "amesema.

Amesema kutokana na mahitaji makubwa ya usafiri, baadhi ya abiria hukubali kulipa zaidi ili wapate kusafiri.

Dk. Kikoyo ameukumbusha Umoja wa  wamiliki wa mabasi yaendayo mikoani(Taboa),kufuata masharti ya leseni zao na kutoza nauli zilizoidhinishwa na  Sumatra.

"Baraza linawahimiza wamiliki, kuwahimiza wafanyakazi wao wanaokata tiketi katika vituo mbalimbali kuwa waaminifu kwa waajiri  na wateja wao,"amesema.

Amesema wananchi wasinunue tiketi kwa wapiga debe au vishoka katika kituo cha mabasi Ubungo au vituo vingine pamoja na kuhakikisha jina na kiwango sahihi alichotoa na kilichoandikwa.

Ameongeza magari yaliyopewa vibali vya muda kusafirisha abiria mikoani yakaguliwe kwa kina kabla ya kukata tiketi.


Kuhusu wanaobeba mizigo katika vitua vya mabasi amesema ‘’ Kwanza mkubaliane bei kabla hajabeba mizigo  pia akupe au akuonyesha kadi yake yenye namba iliyoandikwa kwenye koti lake nyuma, mbele na kwenye toroli lake.’’ 

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search