Waziri Jafo ateta na wakuu wa wilaya...soma habari kamili na matukio360...#share
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
WAKUU wa Wilaya nchini wameagizwa kusimamia kazi zinazofanywa
na Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (Tarura) ili kuleta matokeo
tarajiwa katika kukuza ustawi wa uchumi nchini.
Waziri wa Nchi
Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo katika
kikao cha Wakuu wa Wilaya kuhusiana na kujenga uelewa wa majukumu
ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini(Tarura) katika ukumbi wa Hazina
Dodoma.
Agizo hilo limetolewa leo mjini Dodoma na waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Suleimani Jafo akifungua kikao cha
wakuu wa wilaya nchini.
Jafo amesema “Nawaagiza wakuu wa wilaya nchini kote muende kusiamamia
barabara hizo kwa ukaribu ili barabara zitakazo jengwa ziwe na ubora na
zitakazo dumu kwa muda mrefu,”.
Amewaambia viongozi hao kuwa uanzishwaji wa Tarura utainua chachu
ya
uzalishaji wa mazao kutokana na usafiri wa uhakika kwani mkulima atakuwa na uhakika wakusafirisha mazao, lakini pia itapunguza gharama za
usafiri na kuboresha hali za maisha za watanzania.
Ameeleza kwamba serikali imekuwa na changamoto kubwa ya wakandarasi wanaopatiwa kazi za ujenzi wa barabara kutokuwa waaminifu na kujenga chini ya kiwango, rushwa , hivyo ni kazi ya mkuu wa Wilaya kusimamia ili kubaini mapungufu hayo kwa haraka na kuokoa fedha za Serikali.
uzalishaji wa mazao kutokana na usafiri wa uhakika kwani mkulima atakuwa na uhakika wakusafirisha mazao, lakini pia itapunguza gharama za
usafiri na kuboresha hali za maisha za watanzania.
Ameeleza kwamba serikali imekuwa na changamoto kubwa ya wakandarasi wanaopatiwa kazi za ujenzi wa barabara kutokuwa waaminifu na kujenga chini ya kiwango, rushwa , hivyo ni kazi ya mkuu wa Wilaya kusimamia ili kubaini mapungufu hayo kwa haraka na kuokoa fedha za Serikali.
Amesema kuwa baada ya kuifahamu Tarura ni jukumu lao kuibua maovu
kwa wafanyakazi wanaofanya maovu ili waweze kuchukuliwa hatua za
kinidhamu kwa kufuata sheria na taratibu za utumishi wa umma.
Amesema kuwa Wakuu wa Wilaya ni wawakilishi wa
serikali katika maeneo yao, hivyo wanawajibu wa kusimamia kwa ukaribu
zaidi katika usimamizi wamradi ya Ujenzi wa Barabara nchini.
No comments:
Post a Comment