Everton yazidi kuchanja mbuga, Rooney afanya yake...soma habari kamili na matukio...#share


Na mashirika ya kimataifa
KLABU ya Swansea City imekubali kipigo cha magoli 3-1 kutoka kwa Everton katika mchezo uliopigwa kwenye dimba la Goodsoonpark.
Wachezaji wa Everton wakishangilia goli

Baada ya kupoteza mchezo huo  Swansea wanaendelea kuburuza mkia wakiwa na alama 12, wakiwa  wamecheza 18.

Kunako dakika ya 35 kipindi cha kwanza Swansea ndio walianza kuzifumania nyavu za Everton kwa goli Leroy Johan Fer.

Katika dakika ya 45, mshambuliaji kinda wa Everton Dominic Calvert-Lewin akasawazisha goli hilo baada ya mkwaju wa penati ya Wayne Rooney kuokolewa.


Kiungo Gylfi Sigurdsson akaongeza goli la pili katika dakika ya 64, Wayne Rooney akasawazisha makosa yake kwa kufunga goli la tatu kwa mkwaju wa penati na kufikisha jumla ya magoli 10, msimu huu.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search