Jeshi la Tanzania, Rwanda waunganisha nguvu...soma habari kamili na matukio360..#share


Na Hussein Ndubikile
JESHI la polisi nchini limeingia makubaliano ya kuunganisha nguvu na kushirikiana katika kupambana na kudhibiti uhalifu wa mtandaoni na jeshi la polisi la Rwanda.
IGP, Simon Sirro

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Inspekta Jenerali wa jeshi hilo IGP, Simon Sirro alipokutana na mkuu wa Jeshi la Polisi la Rwanda, Emmanuel Gasana kuangalia utekelezaji wa makubaliano yaliyoingiwa na majeshi hayo mwaka 2013.

Amesema kutokana na jeshi hilo kuwa na uzoefu wa kupambana na uhalifu wameona ni vyema wakaungana nalo kubadilishana na kupata mbinu madhubuti ya kuwakamata wahalifu na   wanaendelea kushirikiana kupambana na dawa za kulevya kwa kufanya operesheni za pamoja mpakani mwa nchi hizo.

" Tunakwenda vizuri kwani kati ya makubaliano tuliyoingia kipindi cha nyuma yametekelezwa ipasavyo nawaeleza wahalifu ambao wako Rwanda na Tanzania hawako salama watafute shughuli nyingine ya kufanya tutawakamata na watafikishwa mbele ya vyombo husika," amesema Sirro.


Amesema lengo la ushirikiano kiulinzi ni kuhakikisha wananchi wanaishi katika hali ya amani na utulivu na wataalam watatoka nchini kwenda Rwanda kupata uzoefu wa kukabiliana na uhalifu huo wa kimtandao.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search