Mashtaka 23 yanayomkabili mhasibu Takukuru yagonga mwamba...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abdulrahim Sadiki
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imetupilia mbali maombi ya upande wa utetezi katika kesi ya utakatishaji fedha na kumiliki mali za bilioni 3.6 kinyume na mshahara inayomkabili aliyekuwa mhasibu wa  Takukuru, Godfrey Gugai.


Maombi ya upande wa utetezi yalilenga kuiomba mahakama hiyo kuyaondoa mashtaka 23 ya utakatishaji fedha yanayomkabili Gugai na wenzake.

Uamuzi wa kuyatupa maombi hayo umetolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya Wakili wa serikali, Peter Vitalis kusema shauri hilo limeitishwa kwa ajili ya uamuzi.

Hakimu Simba amesema mahakama hiyo inatupilia mbali maombi ya utetezi kwa madai mashtaka 23 ya utakatishaji fedha yapo kimakosa katika hati ya mashtaka.

"Hati ya mashtaka ipo sahihi, hivyo natupilia mbali maombi hayo na upande wa Jamhuri unaweza kuendelea na hatua za upelelezi,".

Baada ya kusema hayo aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 28,2017.

Mbali ya Gugai, washtakiwa wengine ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasin Katera.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na makosa 43, kati ya hayo 19 ni ya kughushi, 23 ni utakatishaji fedha na moja ni kumiliki mali zilizozidi kipato halali.

Gugai anakabiliwa na kosa la kumiliki mali kinyume na kipato chake, ambapo alitenda kosa hilo kati ya Januari 2005 na Desemba 2015.

Inadaiwa akiwa jijini Dar es Salaam kama mwajiriwa wa Takukuru alikuwa akimiliki mali za zaidi ya bilioni 3.6 ambazo hazilingani na kipato chake cha awali na cha sasa cha zaidi ya milioni 800, huku akishindwa kuzitolea maelezo.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search